2 Mutaendelea kunitesa mpaka wakati gani, na kunivunjavunja kwa maneno?
Utawinda maneno ya kusema mpaka wakati gani? Fikiri vizuri nasi tutasema.
Kisha Yobu akajibu:
Mara hizi zote kumi mumenitukana. Basi, hamusikii haya kunitendea vibaya?
Lakini ninyi munajua jambo lile vizuri sana! Mbona, basi munasema maneno yasiyokuwa na maana?
Kama vile Mungu anavyoishi, aliyeniondolea haki yangu, Mungu Mwenye Uwezo aliyeifanya nafsi yangu ikuwe na uchungu,
Utasema mambo haya mpaka wakati gani? Mpaka wakati gani maneno yako yatakuwa matupu kama upepo?
Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.
Ninamwambia Mungu, yeye kikingio changu: “Kwa nini umenisahau? Kwa nini niende huko na huko nikiomboleza kwa kuteswa na adui yangu?”
Mwenzangu amemushambulia rafiki yake, amevunja mapatano yake.
Kila magaribi waadui hao wanarudi wakifoka kama imbwa, na kuzungukazunguka katika muji.
Unikinge na shauri baya la waovu, nayo fujo ya watu wabaya.
Maneno ya ovyo yanaumiza kama upanga, lakini kusema kwa mwenye hekima kunaponyesha kidonda.
Ulimi una nguvu ya kuleta uzima na kuua; wanaopenda kuutumia watakula matunda yake.
Watu wale wakalalamika hivi kwa sauti kubwa: “Bwana mutakatifu na mwenye ukweli, mpaka wakati gani utaendelea kungojea kuwahukumu wakaaji wa dunia na kuwaazibu kwa sababu ya kuuawa kwetu?”
Delila alipoendelea kumusumbua sana Samusoni kwa maneno, siku kwa siku na kumwuzi hata akachoka ndani ya roho karibu kufa,