Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 18:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Miguu yake mwenyewe itamutia katika mutego; kila mara anatembea juu ya shimo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 18:8
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Ikikupendeza, ewe mufalme, amri itolewe, watu hawa waangamizwe. Nami ninaahidi, kama utaamuru hivyo, nitatoa kiasi cha kilo elfu kumi za feza iwekwe katika hazina ya mufalme.”


Kule akawaelezea Zeresi, muke wake, na warafiki zake wote mambo yote yaliyomupata. Zeresi na hao warafiki zake wakamwambia: “Ikiwa huyu Mordekayi, ambaye umeanza kupoteza madaraka yako kwa ajili yake ni wa kabila la Wayuda, basi, hautamuweza; atakushinda kabisa.”


Naye, Hamani akauawa pale kwenye muti aliokuwa amemutayarishia Mordekayi. Basi, hasira ya mufalme ikapoa.


Hapo mufalme Ahasuero akamwuliza malkia Esteri: “Ni nani huyo anayesubutu kufanya jambo kama hilo? Yuko wapi mutu huyo?”


Mutego unamukamata kwenye kisigino, kamba inamunasa kabisa.


Mujue kwamba Mungu amenitendea vibaya na kuninasa katika wavu wake.


Kwa hiyo mitego imekuzunguka pande zote, hofu ya rafla imekupata.


Mazao yake yanakuliwa na wenye njaa, hata ngano iliyoota kati ya miiba. Wenye tamaa wananyanganya utajiri wake.


Maangamizi yawapate wao kwa rafla, wanaswe katika mutego wao wenyewe, watumbukie katika shimo lao wenyewe!


kusudi nitangaze sifa zako mbele ya watu wa Sayuni, nipate kushangilia kwa sababu umeniokoa.


Mutu mubaya ananaswa kwa kosa lake, lakini mutu wa haki anaimba na kufurahi.


Mutu mwovu ananaswa kwa uovu wake mwenyewe; anakamatwa na vifungo vya zambi yake mwenyewe.


Woga, mashimo na mitego, hivi ndivyo vinavyowangojea, enyi wakaaji wa dunia.


Mutu atakayekimbia sauti ya woga atatumbukia ndani ya shimo; na mutu atakayetoka ndani ya shimo atanaswa katika mutego. Madirisha ya mbinguni yamefunguliwa, misingi ya dunia inatikisika.


Bwana wetu Yawe anasema: Nitautupa wavu wangu juu yako, nao watu watakuvua humo kwa wavu wangu.


Vilevile inafaa akuwe mutu mwenye kushuhudiwa vizuri na watu wa inje ya kanisa, kusudi asizarauliwe na kunaswa katika mutego wa Shetani.


Lakini wale wanaotaka kuwa watajiri wanaanguka katika majaribu na mitego, na katika tamaa nyingi za upumbafu na mabaya zinazowatumbukiza katika anguko na uharibifu.


Kwa njia hiyo wanaweza tena kupata ufahamu na kuponyoka katika mitego ya Shetani, aliyewanasa na kuwafanya watimize mapenzi yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ