Wakati ule, Daudi aliambiwa kwamba hata Ahitofeli alikuwa mumoja wa waasi waliojiunga na Abusaloma. Lakini Daudi akaomba akisema: “Ee Yawe, ninakuomba uyafanye mashauri ya Ahitofeli yasifanikiwe.”
Abusaloma pamoja na watu wote wa Israeli wakasema: “Shauri la Husayi ni bora kuliko shauri la Ahitofeli.” Wakakataa shauri la Ahitofeli kwa sababu Yawe alikuwa amepanga kulishinda shauri jema la Ahitofeli kusudi aweze kumuletea Abusaloma hasara.
Mufalme wa Aramu akafazaishwa sana na hali hiyo. Akawaita wakubwa wa waaskari wake, akawauliza: “Muniambie ni nani kati yenu anayekuwa upande wa mufalme wa Israeli?”
Kwa maana hekima ya kidunia ni upumbafu mbele ya Mungu. Ni sawa vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Mungu anawanasa wenye hekima katika werevu wao wenyewe.”