Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 17:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Hata hivyo, mutu wa haki anashika njia yake, mutu ambaye hajafanya ubaya kwa mukono wake anazidi kuwa na nguvu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 17:9
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Si ni Abrahamu mwenyewe ndiye aliyesema kwamba huyu ni dada yake? Tena hata Sara mwenyewe alisema kwamba Abrahamu ni kaka yake! Mimi nimefanya nilivyofanya kwa moyo safi na sina kosa.”


Kulikuwa vita ya muda murefu kati ya watu waliokuwa upande wa jamaa ya Saulo, na wale waliokuwa upande wa jamaa ya Daudi. Lakini Daudi alizidi kupata nguvu zaidi na zaidi, wakati upande wa Saulo ulizidi kuwa zaifu zaidi na zaidi.


Yeye anamwokoa mutu asiyekuwa na kosa. Nawe utaokolewa kwa sababu haukutenda mabaya.


Siwezi kabisa kusema kwamba ninyi munasema ukweli. Mpaka kufa kwangu ninasema sina kosa.


Ninashikilia haki yangu, wala sitaiacha; katika zamiri yangu sina cha kunihukumu katika maisha yangu.


kama hatua zangu zimepotoka nao moyo wangu ukafuata tamaa za macho yangu, kama mikono yangu imechafuliwa na zambi,


Wewe umesema hivi: “Mimi niko safi, wala sina kosa. Hakuna ubaya wowote katika moyo wangu.


Kama misingi ikiharibiwa, mutu wa haki atafanya nini?”


Ni mutu wa matendo mema na moyo safi, asiyefuata mambo ya ovyo, wala kuapa kwa uongo.


Ninanawa mikono yangu kuonyesha kama sina kosa, na kuizunguka mazabahu yako, ee Yawe,


Kweli ni kwa bure nimejichunga katika usafi wa moyo, na kujilinda nisitende zambi?


Siku moja tu ndani ya hekalu lako, ni bora kuliko siku elfu pahali pengine; afazali kubakia kwa mulango wa nyumba yako, kuliko kuishi ndani ya nyumba ya waovu.


Wanapopita katika bonde lenye kukauka la Baka, wanalifanya kuwa chemichemi, nazo mvua za kwanza zinalijaza maji.


Wanaendelea wakipata nguvu zaidi na zaidi: watamwona Mungu wa miungu huko Sayuni.


Upepo mukali unapopita na mwovu anatoweka, lakini mwenye haki anaimarishwa milele.


Wenye haki hawataondolewa katika inchi hata kidogo, lakini waovu hawatakaa katika inchi.


Mwenye hekima ni mwangalifu na anaepuka uovu, lakini mupumbafu hajizuizi wala hana uangalifu.


Njia ya wenye haki ni kama mwangaza wa asubui mapema, ambao unaangaza zaidi na zaidi hata muchana kamili.


Wakawaona wanafunzi wake wamoja wakikula chakula na mikono michafu, maana yake, mikono waliyokosa kunawa kufuatana na desturi ya dini yao.


Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia. Musafishe mikono yenu, ninyi wenye zambi! Mutakase mioyo yenu, ninyi wenye nia mbili!


Ninyi ambao kwa imani munalindwa salama kwa nguvu za Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa kwa mwisho wa nyakati.


Watu hawa wametoka kati yetu, lakini hawakukuwa wa kundi letu, na kwa sababu hii wametuacha. Kama wangekuwa wa kundi letu, wangekaa pamoja nasi. Lakini wametuacha kusudi ionekane wazi ya kama hawakukuwa wa kundi letu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ