3 Ee Mungu, ujitoe mwenyewe kuwa rehani kwa ajili yangu maana hakuna mwingine wa kujitoa kwa ajili yangu.
Mimi mwenyewe nitakuwa rehani kwake. Wewe utanidai mimi. Nisipomurudisha umwone kwa macho yako mwenyewe, kosa likuwe juu yangu milele.
Zaidi ya hayo, mimi peke yangu nilijitoa kuwa rehani kwa huyu kijana kwa baba yangu, nikisema: ‘Nisipomurudisha Benjamina kwako, kosa likuwe juu yangu milele.’
Ita sasa, uone kama kuna wa kukuitikia. Ni nani kati ya watakatifu utakayemwita?
Hakuna mwamuzi kati yetu ambaye angetuamua sisi wawili.
Uhakikishe kunisaidia mimi mutumishi wako; usikubali wenye kiburi wanitese.
Anayejitoa kulipia mugeni deni yake atajuta, lakini anayechukia mapatano yale ana usalama.
Mutu asiyekuwa na akili anajitoa rehani kwa deni ya mutu mwingine.
Mutu akiahidi kumukopesha mutu asiyejulikana, unyanganye nguo yake kuwa rehani.
Usikuwe mumoja wa wale ambao wanajitoa rehani kwa madeni ya wengine.
Wakati ule umasikini utakushambulia kama munyanganyi, ukosefu utakufuata kama mwizi mwenye silaha.
Ninalia kama mbaruwayi, ninaugua kama njiwa. Macho yangu yamefifia kwa kuangalia juu. Ee Bwana, ninateseka; ukuwe wewe usalama wangu!
Kwa sababu ya kiapo hiki, Yesu amekuwa kihakikisho kwetu cha agano linalokuwa zuri zaidi.