16 Tazamio langu litashuka nami kuzimu! Tutateremuka wote wawili mpaka kule katika mavumbi!
Kisha Bildadi, wa inchi ya Suhi, akajibu:
Japo alijisikia amejaa nguvu ya ujana, lakini italala pamoja naye katika mavumbi.
Nyuma yake watu wengi wanamusindikiza na wengine wengi sana wanamutangulia. Anapozikwa, udongo unateremushwa polepole.
Siku zangu zinapita mbio kuliko gurudumu la mushonaji, nazo zinafikia mwisho wake bila matumaini.
Kama vile wingu linavyofifia na kutoweka, ndivyo nao watu wanavyoshukia kuzimu bila kurudi.
Ee Yawe, unijibu haraka; maana roho yangu imeregea kabisa! Usinigeuzie mugongo, kusudi nisikuwe kama wale wanaoshuka katika shimo la wafu.
Kwa hiyo Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu! Mifupa hiyo ni mufano wa watu wote wa inchi ya Israeli. Wao, wanasema: Mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yamepotea nasi tumekwisha kabisa.
Maji yalinizunguka na kunisonga; kilindi kilinifikia kila upande, majani ya bahari yakanifunika kichwa.
Tulikuwa tumefikiri kwamba tulihukumiwa kufa. Basi, ilitokea hivi kusudi tusijitegemee sisi wenyewe, lakini tumutegemee Mungu tu anayefufua wafu.