11 Siku zangu zimekwisha, mipango yangu imevunjwa, matazamio ya moyo wangu yametoweka.
Nimevunjika moyo, siku zangu zimekwisha, kaburi langu liko tayari.
Kwa hao watu, usiku ni muchana: wanasema kwamba mwangaza unakaribia giza.
Siku zangu zinapita mbio kuliko gurudumu la mushonaji, nazo zinafikia mwisho wake bila matumaini.
Mwanadamu anapanga mipango yake, lakini neno la mwisho ni la Yawe.
Mutu anaweza kufanya mipango yake, lakini Yawe anaongoza hatua zake.
Katika moyo wa mutu muna mipango mingi, lakini anachokusudia Yawe ndicho kitakachokamilika.
Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.
Nilisema: nikiwa mubichi kabisa, inanipasa niage dunia. Mimi nimepangiwa kwenda katika kuzimu siku zote zilizonibakilia.
Mushauriane pamoja lakini itakuwa bure; mufanye mipango lakini haitawezekana, maana Mungu Yuko Pamoja Nasi.
Nani anayeweza kusema kusudi kitu kifanyike ikiwa Yawe asipoamuru ikuwe hivyo?
Wandugu zangu, ninataka mujue kwamba mara nyingi nilikusudia kuwatembelea, lakini mpaka sasa ninapata vizuizo. Ningetamani kupata matunda ya kazi yangu katikati yenu vilevile, kama inavyokuwa katikati ya watu wa mataifa mengine.