Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 16:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Kama mungekuwa mimi, na mimi ninyi, ningeweza kusema kama ninyi. Ningeweza kutunga maneno juu yenu, na kutikisa kichwa changu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 16:4
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hili ndilo neno Yawe alilosema juu yake: “Watu wa Sayuni wanakuzarau kabisa, watu wa Yerusalema wanakutikisia kichwa kwa kukuchekelea.


Wingi huu wa maneno uachwe tu bila kujibiwa? Mutu wa maneno mengi anaonyesha kwamba hana kosa?


Ningeweza kuwatia moyo kwa maneno yangu, na maneno yangu ya faraja yangewatuliza.


Yobu anafungua kinywa kusema maneno matupu, anazidisha maneno bila akili.


Anayekataa kutendea mema rafiki yake, anakataa kumwogopa Mungu Mwenye Uwezo.


Watu wananichekelea; wanaponiona wanatikisa vichwa vyao kwa kunizarau.


Lakini mimi ni mududu tu, wala si mutu; nimetukaniwa na kuzarauliwa na watu.


Wote wanaoniona wananichekelea; wananizomea na kutikisa vichwa vyao.


Umetupotezea heshima mbele ya jirani zetu, nao wanatuchekelea na kutuzarau.


Kwenye kuwa maneno mengi hakukosekani makosa, lakini aneyezuia ulimi wake ana akili.


Mupumbafu anasema maneno mengi. Mwanadamu hajui yatakayokuwa, wala yale yatakayotukia nyuma yake.


basi huu ndio ujumbe wa Yawe juu ya huyo mufalme: Watu wa Sayuni wanakuzarau kabisa, Watu wa Yerusalema wanakutikisia kichwa kwa kukuchekelea.


Wameifanya inchi yao kuwa kitisho, kuwa kitu cha kuzomewa siku zote. Kila mutu anayepita huko anashangaa na kutikisa kichwa chake.


Ee Moabu, si ulimuchekelea Israeli! Ulimuhesabu kama mwenzake na wanyanganyi hata ukakuwa unatikisa kichwa chako kila mara uliposema juu yake.


Wapita njia wote wanakuchekelea; wanakupigia muunzi, ee Yerusalema, wakitikisa vichwa vyao kwa mazarau na kusema: Huu ndio ule muji uliofikia ukamilifu wa uzuri, muji uliokuwa furaha ya dunia nzima?


Basi huu ndio muji uliojivuna na kuishi kwa usalama, muji uliojisemesha: Ni mimi tu, hakuna mwingine! Jinsi gani umekuwa mutupu na makao ya nyama wa pori! Kila mutu anayepita karibu atauzomea na kuuzarau.


“Basi jambo lolote munalotaka wengine wawatendee, ninyi mulitende kwao vilevile, kwa maana kile ndicho kifungo cha Sheria ya Musa na mafundisho ya manabii.


Mufurahi pamoja na wenye kufurahi. Mulie pamoja na wenye kulia.


Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vingine vyote vinaugua pamoja nacho. Kiungo kimoja kikiheshimiwa, viungo vingine vyote vinafurahi pamoja nacho.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ