16 Kama nikiweza kwa hiyo nitakuwa nimeshinda, maana mutu mwovu hawezi kwenda mbele yake.
Musikilize kwa uangalifu maneno yangu, maelezo yangu yatue katika masikio yenu.
Pale, mutu wa usawa anaweza kujitetea. Mungu, mwamuzi wangu angeamua kuwa sina kosa milele.
Macho ya Mungu yanachunguza mienendo ya watu; yeye anaziona hatua zao zote.
Waovu wanapenda kukasirika; hawamwombi musaada anapowafunga.
Ndivyo wote wanaomusahau Mungu wanavyokuwa. Tumaini la wasiomwamini Mungu litapotea.
Yawe ni nguvu yangu kubwa; yeye mwenyewe ndiye wokovu wangu.
Ninakushukuru, ee Yawe, kwa kunijibu; kwa sababu wewe ni wokovu wangu.
Zaburi ya Daudi. Yawe ni mwangaza wangu na wokovu wangu, ni nani nitakayemwogopa? Yawe ni mulinzi wa maisha yangu, sitamwogopa mutu yeyote.
Yawe ananijalia nguvu na uwezo, yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa. Yeye ni Mungu wangu nami nitamusifu; ni Mungu wa baba yangu nami nitamutukuza.
Wenye zambi katika Sayuni wanaogopa, wasiomwamini Mungu wanatetemeka na kusema: Nani anayeweza kuvumilia moto huu mukali? Nani anayeweza kuvumilia ndimi za moto usiozimika?
Kweli tumedanganyika sana kwa kutambikia huko kwenye vilima, hakika wokovu wa Israeli unatoka kwake Yawe, Mungu wetu.
Kwa maana Bwana ametuagiza hivi: ‘Nimekuweka kuwa mwangaza wa mataifa, kusudi watu wapate kuokolewa katika dunia yote.’ ”