Lakini sasa watu wananichekelea, tena watu wanaokuwa wadogo kuliko mimi; watu ambao niliwaona baba zao hawafai hata kuwahesabu kama imbwa wangu wakilinda kondoo.
Ee Yawe, wewe umenidanganya, nami kweli nimedanganyika; wewe una nguvu kuliko mimi, nawe umeshinda. Nimekuwa mutu wa kuchekelewa kila siku, kila mutu ananizarau.
Nao wakasokota taji na tawi lenye miiba na kumuvalisha nalo kwenye kichwa chake. Wakaweka tete katika mukono wake wa kuume, wakapiga magoti mbele yake na kumuchekelea, wakisema: “Jambo, Mufalme wa Wayuda!”
Nao wakaanza kumuchekelea. Halafu Yesu akawaondosha wote inje, akawakamata wazazi wa yule mutoto na wanafunzi wake watatu, akaingia katika chumba pahali mutoto alipokuwa.