“Lakini, ee Mungu kweli utakaa humu katika dunia na wanadamu, ikiwa hata mbingu zenyewe, wala mbingu za mbingu za juu sana hazikutoshi? Namna gani nyumba hii ambayo nimejenga itakutoshelea?
Ni nani aliyepanda juu mbinguni na kushuka chini? Ni nani aliyekamata upepo katika mukono? Ni nani aliyefunga maji katika kitambaa? Ni nani aliyeweka mipaka yote ya dunia? Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwana wake? Uniambie kama unajua!