Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 11:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Unaweza kuvumbua siri za Mungu na kujua ukomo wa Mungu Mwenye Uwezo?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 11:7
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tunajua kwamba Mungu yuko kule juu mbinguni; Angalia jinsi nyota za juu kabisa zinavyokuwa mbali!


Ikiwa haya ni machache tu ya matendo yake, ni minongono tu tunayosikia juu yake, nani anayeweza kujua ukubwa wa nguvu yake?


Nitawafundisha jinsi kitendo cha Mungu kinavyokuwa, sitawaficha mipango ya Mungu Mwenye Uwezo.


Lakini Yobu, ninakuambia pale umekosa. Mungu ni mukubwa kuliko mwanadamu.


Kwa nini unashindana naye, ukisema hatajibu ulizo lako moja?


Basi uangalie mbingu! Angalia mawingu yanayokuwa juu kuliko wewe!


Mungu ni mukubwa sana hata hatuwezi kumujua; muda wa maisha yake hauchunguziki.


Mungu Mwenye Uwezo asiyeweza kufikiwa na mutu, uwezo na haki yake ni mukubwa. Amejaa haki wala hapotoshi sheria hata kidogo.


Mungu anapiga radi ya ajabu kwa sauti yake, anafanya mambo makubwa tusiyoweza kuyaelewa.


Ulisema kwamba nilivuruga mipango yako bila akili. Kweli nilitamka kitu ambacho sikuelewa, mambo ya ajabu sana kwangu ambayo sikukuwa ninayajua.


yeye anayetenda mambo makubwa yasiyochunguzika, anayetenda maajabu yasiyohesabika.


Ufahamu wako unapita akili yangu; ni mukubwa sana, siwezi kuuelewa.


Yawe ni mukubwa, anastahili sifa nyingi; ukubwa wake hauwezi kuchunguzika.


Kishindo cha ngurumo yako kilitokea katika zoruba, umeme wako ukaangaza ulimwengu, dunia ikatikisika na kutetemeka.


Ni nani aliyepanda juu mbinguni na kushuka chini? Ni nani aliyekamata upepo katika mukono? Ni nani aliyefunga maji katika kitambaa? Ni nani aliyeweka mipaka yote ya dunia? Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwana wake? Uniambie kama unajua!


Mungu amefanya kila kitu kikuwe kizuri kwa wakati wake. Ameweka ndani ya moyo wa mwanadamu mawazo juu ya muda usiokuwa na mwisho, lakini mutu hawezi kuelewa mwanzo na mwisho wa matendo ya Mungu.


Jinsi gani mwanadamu ataweza kutambua maana ya maisha? Jambo hilo ni zito na gumu sana kwetu.


Ninyi hamujui bado? Hamujapata kusikia? Yawe ndiye Mungu wa milele; yeye ndiye Muumba wa kila kitu katika dunia. Yeye haregei hata kidogo wala kuchoka. Maarifa yake hayachunguziki.


“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


Utajiri wa Mungu, hekima na ufahamu wake ni vikubwa kupita kipimo! Hakuna anayeweza kuvumbua kusudi lake wala kuelewa mipango yake!


Lakini Mungu ametufunulia sisi siri yake kwa njia ya Roho wake. Maana Roho anachunguza vitu vyote, hata mipango ya Mungu inayofichwa kabisa.


Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Ni nani anayejua mawazo ya Bwana? Ni nani anayeweza kumushauria?” Lakini sisi tuko na mawazo yanayotoka kwa Kristo.


Mimi ni mudogo kuliko watu wote wa Mungu, lakini Mungu amenijalia neema ya kutangaza kwa watu wa mataifa mengine Habari Njema ya baraka za Kristo zisizoweza kuhesabiwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ