3 Kupapayuka kwako kutanyamazisha watu? Kama ukichekelea watu, hakuna atakayekupatisha haya?
Nilikuwa mutu wa kumwomba Mungu na kupata jibu lake. Sasa, watu wananichekelea. Wanachekelea mutu mukamilifu, mwenye haki.
Lakini ninyi munapakaa uongo chokaa, ninyi wote ni waganga wasiofaa kitu.
Akiwachunguza, ninyi mutapona? Au munazani munaweza kumudanganya Mungu kama watu?
Kweli wanaonichekelea wamenizunguka, matusi yao yananizuiza kulala.
Munivumilie, nami nitasema, na nikisha sema muendelee kunichekelea.
Nani basi, anayeweza kuhakikisha kwamba mimi ni mwongo na kuonyesha kwamba maneno yangu si kweli?
Ni nani anayekuwa kama Yobu ambaye kwake mazarau ni kama kunywa maji?
Walinichekelea, walinisagia meno.
uwakimbize hao kwa zoruba yako, na kuwatisha kwa upepo wako mukali!
Mimi sikuikaa pamoja na wanaojifurahisha, wala sikufurahi pamoja nao. Niliikaa peke yangu nikilemewa na nguvu yako; kwa maana ulinijaza hasira yako.
Kama mutu hataki kushika maagizo tunayowatolea katika barua hii, mumwangalie vizuri mutu yule, musishirikiane naye, kusudi apate haya.
Ufundishe maneno ya kweli watu wasiyoweza kubishia, hata wale wanaokupinga wapate haya kwa kukosewa na neno baya la kusema juu yetu.
Wao waliwaambia: “Katika siku za mwisho, kutakuja watu watakaowachekelea, wakiishi kwa kufuata tamaa zao mbaya.”