Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 10:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Wewe unajua kwamba mimi sina kosa, na hakuna wa kuniokoa toka katika mikono yako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 10:7
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kama mimi ni mwovu, ole wangu! Kama mimi ni mwenye haki, siwezi kujisifu; maana nimejaa haya, nikiangalia mateso yangu.


Wewe unasema: “Masemi yangu ni safi, mimi sina kosa mbele ya Mungu.”


Maneno yangu nimeyatarisha jinsi inavyofaa. Ninajua kwamba sina kosa.


Lakini yeye anajua njia ninayofuata; atakapomaliza kunipima nitatoka mule safi kama zahabu.


Ninamufuata kabisa; njia yake nimeishikilia wala sikugeuka pembeni.


Upepo ule unamufunika bila huruma; anajaribu kukimbia lakini mbio za bure.


nitafanya nini basi Mungu atakaposimama mbele yangu? Akinichunguza, nitamujibu nini?


Heri kungekuwa mutu wa kunisikiliza! Ninaweza kutia sahihi yangu katika kila neno nililosema. Mungu Mwenye Uwezo anijibu! Heri mashitaki waadui zangu wanayonitolea yangeandikwa!


Basi hawa watu watatu: Elifasi, Bildadi na Zofari, wakaacha kumujibu Yobu kwa vile alijiona kuwa mwenye haki.


Wewe umesema hivi: “Mimi niko safi, wala sina kosa. Hakuna ubaya wowote katika moyo wangu.


Unataka kweli kugeuza hukumu yangu, kuniona nina kosa kusudi wewe usikuwe na kosa?


Yawe alipomaliza kuongea na Yobu, akamwambia Elifasi wa inchi ya Temani: “Kasirani yangu imewaka juu yako na warafiki zako wawili maana hamukusema ukweli juu yangu kama vile mutumishi wangu Yobu alivyofanya.


Yeye akitwaa kitu kwa rafla, nani anayeweza kumuzuia? Nani anayeweza kumwuliza: “Unafanya nini?”


Mimi ni mukamilifu. Siangalii nafsi yangu. Ninachukia maisha yangu.


Yote ni mamoja, kwa hiyo ninasema: Mungu anawaangamiza wakamilifu na waovu.


Maana Yawe anashugulikia njia ya watu wa haki; lakini njia ya waovu itaangamia.


Wewe unajua kabisa moyo wangu; umenifikia usiku kunichunguza, umenitia katika majaribu; haukuona uovu ndani yangu, sikusema kitu kisichofaa.


“Mufikiri vizuri jambo hili, enyi musionijali, kama sivyo nitawaangamiza, wala hakuna atakayewaokoa.


Kama si vile, watakuja kunirarua kama simba, kunipasua vipandevipande wala hakuna wa kuniokoa.


Mimi ni Mungu na nitakuwa Mungu siku zote. Hakuna anayeweza kuepuka nguvu yangu; hakuna anayeweza kupinga ninayofanya.


Basi, mutakaposikia tena sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, muko tayari kuinama chini na kuiabudu sanamu niliyotengeneza? Kama mukikataa, mutatupwa mara moja katika furu la moto mukali. Ni mungu gani anayeweza kuwaokoa katika mikono yangu?


Hakujua kwamba ni mimi niliyemupa ngano, divai na mafuta, niliyemujalia feza na zahabu kwa wingi, ambazo alimupelekea mungu Bali.


Maana mimi nitakuwa kama simba kwa Efuraimu, kama simba mukali kwa watu wa Yuda. Mimi mwenyewe nitawararua na kuondoka, nitawakamata na hakuna atakayewaokoa.


Kisha Yesu akamwuliza mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?” Basi Petro akauzika kwa sababu Yesu alimwuliza mara ya tatu kama anamupenda. Kwa hiyo akamujibu: “Bwana, unajua yote; unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia: “Tunza kondoo wangu.


Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.


Muone kwamba mimi ni Mungu na wala hakuna mwingine isipokuwa mimi. Mimi ninaua na kuweka uzima, ninaumiza na kuponya, na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote toka katika mikono yangu.


Ninyi ni washuhuda wetu, na Mungu vilevile anashuhudia kwamba tulipokaa kati yenu ninyi waamini, tuliishi katika utakatifu na haki, na bila kosa.


“Mungu wa miungu ndiye Yawe! Mungu wa miungu ndiye Yawe! Yeye anajua kwa nini tumefanya hivyo. Na Waisraeli wote watajua vilevile! Kama huu ni uasi au ni ukosefu wa imani kwa Yawe basi, yeye aache kutuokoa leo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ