Farasi hao walipotokea walikuwa na hamu sana ya kwenda kuichunguza dunia. Naye malaika akawaambia: Basi! Muende muichunguze dunia. Basi, wakaenda na kuichunguza dunia.
Basi yule nyoka mukubwa akafukuzwa. Yeye ndiye yule nyoka wa zamani anayeitwa “Mwovu” au “Shetani,” anayedanganya watu wote. Akatupwa katika dunia pamoja na wamalaika zake.
naye atakwenda kuwadanganya watu wa mataifa wanaokuwa katika pande zote za dunia, ndio wanaoitwa Gogi na Magogi. Shetani atawakusanya kwa kupigana vita, nao watakuwa wengi kama vile muchanga wa bahari.