Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 9:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 na kumwambia: “Kwenda unawe uso katika kisima cha Siloamu” (maana ya jina hili ni “Aliyetumwa”). Basi yule kipofu akaenda na kunawa uso, akarudi akiwa mwenye kuona.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 9:7
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mulango wa Chemichemi ukajengwa upya na Salumu mwana wa Koli-Hoze, mukubwa wa wilaya ya Misipa. Akaufunika, akauweka mulango kwa nafasi yake, akatia vyuma na vifungio vyake. Kwenye Kisima cha Sela akajenga ukuta unaokuwa karibu na bustani ya kifalme mpaka kwenye ngazi zinazoshuka toka muji wa mufalme Daudi.


anawafungua vipofu macho. Yawe anawainua waliogandamizwa; anawapenda watu wa haki.


Halafu Yawe akamwuliza: “Ni nani aliyeumba kinywa cha mutu? Ni nani anayemufanya mutu kuwa bubu au kiziwi? Aone au akuwe kipofu? Si mimi Yawe?


Macho ya wanaoona hayatapofushwa tena, masikio ya wanaosikia yatabaki wazi.


Hapo vipofu wataona tena, na viziwi watasikia tena.


Utayafungua macho ya vipofu, utawafungua wafungwa toka katika kifungo, utawaweka huru wale waliofungwa katika giza.


Muwalete mbele watu hao, ambao wana macho lakini hawaoni, wana masikio lakini hawasikii!


Kwa sababu watu hawa wameyakataa maji ya Siloa yanayotiririka polepole, wakatetemeka mbele ya mufalme Resini na mufalme Peka mwana wa Remalia,


vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanapata kusikia, wafu wanafufuliwa na Habari Njema inahubiriwa kwa wamasikini.


Vilevile munazani kwamba wale watu kumi na wanane waliokufa munara ulipowaangukia kule Siloamu, walikuwa wakosaji kuliko wakaaji wengine wote wa Yerusalema?


Ndio utakaowaangazia mataifa, na kuleta utukufu kwa watu wako Waisraeli.”


Kwa upande wangu, nilichaguliwa na Mungu na kutumwa naye katika dunia. Basi namna gani munasema kwamba ninamutukana Mungu kwa sababu nilisema kwamba mimi ni Mwana wa Mungu?


Lakini wengine kati yao wakasema: “Yeye aliyeponyesha kipofu, asingeweza kuzuia mutu huyu asikufe?”


Akajibu: “Mutu yule anayeitwa Yesu alifanya matope kidogo na kuyapakaa kwa macho yangu, na kuniambia kwamba niende kunawa uso katika kisima cha Siloamu. Nami nikaenda, nikanawa, na halafu nikapata kuona.”


Kisha Yesu akasema: “Nimekuja katika dunia kusudi hukumu ipate kufanyika; maana yake vipofu wapate kuona, nao wanaoona wapate kuwa vipofu.”


kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’


Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.


Lakini wakati uliopangwa ulipotimia, Mungu akamutuma Mwana wake: akazaliwa na mwanamuke na kuishi chini ya uongozi wa Sheria,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ