37 Yesu akamwambia: “Umemwona, na ni yeye anayesema nawe sasa.”
Yawe ni rafiki ya wale wanaomwabudu; yeye anawajulisha agano lake.
Ninyi mumeona mambo mengi, lakini hamuelewi kitu. Masikio yenu yako wazi, lakini hamusikii kitu!
Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.
Yesu akamujibu: “Mimi ninayesema nawe, ndiye.”
Kama mutu akitaka kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu, au kama ninasema kwa mamlaka yangu mwenyewe.
Basi yule mutu akasema: “Bwana, ninaamini.” Naye akamwabudu Yesu.