Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 9:35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

35 Yesu akapata habari kwamba yule aliyekuwa kipofu amefukuzwa. Yesu alipokutana naye, akamwuliza: “Unamwamini Mwana wa Mutu?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 9:35
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme anasema: “Nitatangaza amri ya Yawe. Mungu aliniambia: ‘Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.


Hata kama wazazi wangu wakinitupa, Yawe atanipokea kwake.


Basi wanafunzi waliokuwa ndani ya chombo wakapiga magoti mbele ya Yesu, wakisema: “Kweli wewe ni Mwana wa Mungu!”


Simoni Petro akamujibu: “Wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu Mwenye Uzima.”


Shetani akamufikia na kumwambia: “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yageuke kuwa mikate.”


Huu ndio mwanzo wa Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.


Hakuna mutu aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini Mwana wa pekee anayekuwa Mungu, anayeishi pamoja na Baba, huyu ndiye aliyemutambulisha kwetu.


Mimi nimeona mambo haya, nami ninashuhudia kwamba huyu ndiye Mwana wa Mungu.”


Kwa upande wangu, nilichaguliwa na Mungu na kutumwa naye katika dunia. Basi namna gani munasema kwamba ninamutukana Mungu kwa sababu nilisema kwamba mimi ni Mwana wa Mungu?


Akamujibu: “Ndiyo, Bwana, ninaamini kwamba wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu, yule aliyepaswa kuja katika dunia.”


Toma akamujibu: “Bwana wangu na Mungu wangu!”


Lakini hii imeandikwa kusudi mupate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mupate uzima katika jina lake.


Anayemwamini Mwana yuko na uzima wa milele. Anayekataa kumwamini Mwana hatapata uzima; atakaa akipatwa na kasirani ya Mungu.”


Kisha Yesu akamukuta mutu yule ndani ya hekalu, akamwambia: “Angalia, sasa umepona. Basi usifanye zambi tena, kusudi jambo baya zaidi lisikufikie.”


Na sasa tunaamini na kujua kwamba wewe ni Mutakatifu wa Mungu.”


Wazazi wake walisema hivi kwa sababu waliogopa wakubwa wa Wayuda. Wakubwa wale walikuwa wamekwisha kupatana kwamba mutu yeyote anayesadiki kuwa Yesu ndiye Kristo, atatengwa asiingie katika nyumba ya kuabudia.


Wakamujibu: “Wewe, uko mwenye zambi kabisa tangu kuzaliwa kwako! Unataka kutufundisha?” Halafu wakamufukuza inje.


Walipokuwa wakiendelea na safari, wakafika kwenye nafasi moja kwenye maji, yule mukubwa akasema: “Hapa kuna maji. Ni kitu gani kinachonizuiza nisibatizwe?” [


Filipo akamwambia: “Kama unaamini kwa moyo wako wote, unaweza kubatizwa.” Yule mukubwa akamujibu: “Ninaamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.”]


Na bila kukawia akaanza kuhubiri katika nyumba za kuabudia, akitangaza kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.


Isaya kwa uhodari anaongeza kusema maneno haya: “Nimepatikana kwa watu wasionitafuta, nimejifunua kwa watu wasioniuliza.”


Kila mutu anayesema kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu anaungana naye, na mutu yule anaungana na Mungu.


Yule anayemwamini Mwana wa Mungu yuko na ushuhuda huu ndani yake. Lakini yule asiyemwamini Mungu, amemufanya Mungu kuwa mwongo, maana hakuaminia ushuhuda Mungu aliotoa juu ya Mwana wake.


Ninawaandikia maneno yale, ninyi wenye kuamini kwa jina la Mwana wa Mungu, mupate kujua kwamba muko na uzima wa milele.


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


Ni nani anayeshinda dunia? Ni yule anayeamini kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.


Kwa sababu hiyo wakati nitakapokuja, nitaonyesha wazi mambo yote anayotenda akitusingizia sisi maneno mabaya. Lakini hatosheki na mambo yale, yeye mwenyewe anakataa kukaribisha wandugu wale wanaokuwa katika safari. Na wale wanaotaka kuwakaribisha, anawakataza na kuwafukuza katika kanisa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ