Kama vile hauwezi kujua jinsi uzima unavyoingia katika mifupa ya mutoto katika tumbo la mama yake, vilevile hauwezi kuelewa matendo ya Mungu, aliyefanya kila kitu.
Akajibu: “Mutu yule anayeitwa Yesu alifanya matope kidogo na kuyapakaa kwa macho yangu, na kuniambia kwamba niende kunawa uso katika kisima cha Siloamu. Nami nikaenda, nikanawa, na halafu nikapata kuona.”
Kwa hiyo Wafarisayo nao wakamwuliza namna gani alivyopata kuona. Naye akawaambia: “Alinipakaa matope kidogo kwa macho, nami nikanawa uso na sasa ninaona.”
Lakini hatujui kilichotokea hata anaona sasa, wala hatujui ni nani aliyemuponyesha macho. Yeye ni mutu muzima. Mumwulize yeye mwenyewe, naye atawaelezea maneno yake.”