Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 8:59 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

59 Kwa ajili ya hii, wakaokota mawe kwa kumutupia. Lakini Yesu akajificha na kutoka ndani ya hekalu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 8:59
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha wakawapiga kwa kuwapofusha macho wanaume wote waliokuwa kwa mulango, wakubwa na wadogo, hata wakataabika kwa kutafuta ule mulango, nao hawakuupata.


Mutu yeyote akuwe ni mwenyeji au mugeni anayemutukana Yawe, wote pamoja watamwua kwa kumupiga mawe.


Wafarisayo wakaondoka pale na kwenda kufanya shauri la kumwua Yesu.


Halafu, macho yao yakafumbuliwa, wakamutambua. Lakini yeye akatoweka, nao hawakumwona tena.


Kwa sababu hii Yesu hakutembea tena akijionyesha waziwazi kati ya Wayuda. Kisha akajiendea pamoja na wanafunzi wake katika inchi iliyokuwa karibu na jangwa katika muji unaoitwa Efuraimu. Nao wakabaki kule.


Wanafunzi wakamwambia: “Mwalimu, hakujapita siku nyingi tokea pale Wayuda walipotaka kukutupia mawe, na sasa unataka kwenda tena kule!”


Basi muaminie mwangaza ule wakati mungali nao, kusudi mukuwe watu wa mwangaza.” Yesu alipokwisha kusema maneno hayo, akajiendea na kujificha mbali na lile kundi.


Pilato akawaambia: “Ninyi wenyewe mumukamate na mumuhukumu kufuatana na sheria yenu.” Wakamujibu: “Sisi hatuna ruhusa ya kuua mutu.”


Lakini mutu yule aliyeponyeshwa hakujua ni nani, kwa maana Yesu alikuwa amekwisha kuondoka katikati ya kundi kubwa la watu waliokuwa pale.


Yesu alipokuwa akipita katika njia, akaona mutu mumoja aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa kwake.


Basi wale wajumbe wakafunga masikio yao, wakapiga kelele kwa nguvu na kumurukia wote pamoja.


Sasa, Daudi alikuwa katika matatizo makubwa kwa sababu watu wake walikuwa na uchungu katika roho zao kwa kupoteza watoto wao. Kwa hiyo wakakuwa wakitaka kumupiga mawe. Lakini Daudi alijipa moyo kwa kumutegemea Yawe, Mungu wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ