Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 8:56 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

56 Baba yenu Abrahamu alishangilia akitumainia kuona siku ya kuja kwangu; na wakati alipoiona, alifurahi.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 8:56
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kutokana na wazao wako mataifa yote katika dunia yatabarikiwa kwa sababu wewe umeitii amri yangu.”


Kweli ninawaambia: manabii wengi na wenye haki wengi walitamani kuona mambo munayoona, lakini hawakuyaona, na kusikia maneno munayosikia, lakini hawakuyasikia.


Kwa maana ninawaambia: manabii wengi na wafalme walitamani kuona mambo munayoyaona, lakini hawakuyaona, na kusikia maneno munayoyasikia, lakini hawakuyasikia.”


Yesu akawajibu: “Nimekwisha kuwaambia ninyi, lakini hamusadiki. Matendo ninayofanya kwa mamlaka ya Baba yananishuhudia mimi.


Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Abrahamu. Lakini munatafuta kuniua, kwa sababu munakataa kukubali mafundisho yangu.


Wakamujibu: “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia: “Kama mungekuwa watoto wa Abrahamu, basi mungefanya matendo yale Abrahamu aliyofanya.


Watu hawa wote walikufa katika imani pasipo kupokea mambo Mungu aliyoahidi. Lakini waliyaona kwa mbali na kuyafurahia, wakikubali kwamba walikuwa wageni na wasafiri katika dunia.


Watu hawa wote walishuhudiwa vizuri na Mungu kwamba wamemupendeza kwa njia ya imani yao. Lakini hawakupokea mambo yale Mungu aliyowaahidia,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ