Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 8:48 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

48 Wayuda wakamujibu: “Sisi tulikuwa na haki ya kusema kwamba wewe ni Musamaria na kwamba uko na pepo.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 8:48
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe, Mukombozi na Mutakatifu wa Israeli, anamwambia hivi yule anayezarauliwa sana, yule anayechukiwa na mataifa, na ambaye ni mutumishi wa watawala: Wafalme wataona nao watasimama; wakubwa watainama na kuabudu kwa heshima ya Yawe ambaye anatimiza ahadi zake, kwa heshima ya Mutakatifu wa Israeli ambaye amekuchagua wewe.


Alizarauliwa na kukataliwa na watu. Alikuwa mutu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mutu wa kuchukiza kwa watu; alizarauliwa na tukamwona si kitu.


Lakini inatosha kwa mwanafunzi kufanana na mwalimu wake na mutumishi kufanana na bwana wake. Ikiwa wanamwita mukubwa wa jamaa Belzebuli, hawatakosa kuwaita watu wa jamaa yake kwa majina mabaya zaidi.


Hao ndio wanafunzi kumi na wawili Yesu aliowatuma, akiwaagiza mambo haya: “Musiende katika inchi za watu wa mataifa mengine wala musiingie katika muji wowote wa Samaria.


Kwa maana Yoane alikuja, alifunga kula chakula na kunywa, nao wakasema: ‘Yuko na pepo!’


Lakini wakati Wafarisayo waliposikia maneno yale, wakasema: “Ni Belzebuli, mukubwa wa pepo ndiye anayemupa mutu huyu uwezo wa kufukuza pepo.”


Kwa hiyo ninawaambia: watu wataweza kusamehewa zambi zote wanazofanya na matusi yao yote. Lakini mutu anayetukana Roho Mutakatifu hatasamehewa.


Ninyi wanafiki! Isaya alitabiri vema juu yenu, wakati aliposema maneno haya:


Huu ndio ushuhuda wa Yoane kwa makuhani na Walawi waliotumwa na Wayuda kutoka Yerusalema kumwuliza kwamba yeye ni nani.


Wengi kati yao wakasema: “Yuko na pepo! Kweli ni mwenda-wazimu! Sababu gani munamusikiliza?”


Munaniita ‘Mwalimu’ na ‘Bwana,’ na munasema kweli, maana ni vile ninavyokuwa.


Basi yule mwanamuke Musamaria akamwambia Yesu: “Namna gani wewe Muyuda unaweza kuniomba mimi Musamaria maji ya kunywa?” (Wayuda hawakukuwa na ushirika na Wasamaria.)


Watu wale wakajibu: “Wewe uko na pepo. Nani anatafuta kukuua?”


Wakubwa wa Wayuda wakaulizana: “Yeye anasema kwamba hatuwezi kufika pahali anapokwenda; maana yake atakwenda kujiua?”


Halafu Wayuda wakamwambia: “Sasa tunajua hakika kwamba uko na pepo! Abrahamu amekufa, na manabii wamekufa vilevile, nawe unasema kwamba mutu akishika maneno yako, hatakufa hata milele.


Kwa maana hata Kristo hakufanya mambo yanayomupendeza mwenyewe sawa vile ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Matusi wanayokutukana, yananiangukia.”


Basi tumwendee mbali na kambi, tukikubali kuzarauliwa kama vile yeye alivyozarauliwa.


Si wewe unaamini kwamba kuna Mungu mumoja? Ni vizuri! Hata pepo wanaamini vile, nao wanatetemeka kwa woga.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ