wala si wote wanaotoka katika uzao wa Abrahamu, ndio watoto wa kweli wa Abrahamu. Kwa kuwa Mungu alimwahidia Abrahamu: “Ni kwa njia ya Isaka utapata wazao watakaoitwa wako.”
Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.
Nimewaandikia ninyi watoto, kwa sababu mumemujua Baba. Ninawaandikia ninyi wababa, kwa sababu mumemujua yule aliyekuwa tangia mwanzo wa vitu vyote. Ninawaandikia ninyi vijana, kwa sababu muko na nguvu na Neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mumemushinda yule Mwovu.