Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 8:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: kila mutu anayefanya zambi ni mutumwa wa zambi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 8:34
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hakuna mutu aliyekusudia kutenda maovu mbele ya Yawe kama Ahabu, ambaye alishawishiwa na Yezebeli, muke wake.


Mutu mwovu ananaswa kwa uovu wake mwenyewe; anakamatwa na vifungo vya zambi yake mwenyewe.


Kweli ninawaambia: kwa muda wote mbingu na dunia vitakapokuwa vingali, hakuna hata herufi moja wala nukta moja ya Sheria itakayoondoshwa mpaka yote yatimie.


Yesu akamujibu: “Kweli, kweli ninakuambia: mutu hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu asipozaliwa mara ya pili.”


Kwa maana ninaona kwamba umejaa uchungu sana nawe umefungwa na zambi.”


Basi musiache tena zambi kutawala katika mwili wenu wa kufa, hata mupate kufuata tamaa zake mbaya.


Munajua hakika kwamba mukijitoa wenyewe kwa mutu fulani kuwa watumwa wake na kulazimishwa kumutii, munakuwa kweli watumwa wa yule munayemutii. Ikiwa ni utumwa wa zambi, mwisho wake ni kifo; ikiwa ni kumutii Mungu, mwisho wake ni maisha ya haki.


Kwa maana tunajua kwamba ule utu wetu wa zamani ulitundikwa pamoja na Kristo, kusudi tusitawaliwe tena na hiyo tabia ya zambi na tusikuwe tena watumwa wa zambi.


Tunajua kwamba Sheria inaelekea maisha ya kiroho, lakini mimi ni mutu wa kimwili, kwa maana nimeuzishwa kama vile mutumwa wa zambi.


Mungu ashukuriwe kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo! Basi hivi kwa upande mumoja ninatumikia sheria ya Mungu kwa akili yangu, lakini kwa upande mwingine ninatumikia sheria ya zambi kwa hali yangu ya kimwili.


siku moja viumbe hivi vitawekwa huru toka katika utumwa wa uharibifu na kushiriki katika uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.


Mulikuwa mukiishi kufuatana na mwenendo mubaya wa dunia hii. Mulitii mutawala wa roho zenye uwezo wa anga anayetawala sasa watu wasiomutii Mungu.


Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.


Wanawaahidi watu wengine kwamba watakuwa huru ijapokuwa wao wenyewe ni watumwa wa upotovu. Kwa maana kila mutu ni mutumwa wa jambo lolote linalomutawala.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ