Yawe akamwambia Abramu: “Ujue hakika kwamba wazao wako watakaa kama wageni katika inchi isiyokuwa yao, watakuwa watumwa na watateswa kwa muda wa miaka mia ine.
Haukutuacha tuishi katika utumwa ingawa tulikuwa watumwa. Uliwafanya wafalme wa Persia wakuwe wema kwetu na kuturuhusu tuishi na kuijenga nyumba yako iliyokuwa imebomoka, na ukatufanya tukae salama hapa Yuda na Yerusalema.
Basi muonyeshe kwa njia ya matendo kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Musianze tu kujisemesha kwamba Abrahamu ndiye babu yenu. Ninawaambia kwamba Mungu anaweza kugeuza mawe haya kuwa watoto wa Abrahamu!
wala si wote wanaotoka katika uzao wa Abrahamu, ndio watoto wa kweli wa Abrahamu. Kwa kuwa Mungu alimwahidia Abrahamu: “Ni kwa njia ya Isaka utapata wazao watakaoitwa wako.”
Kila mara Yawe alipowapelekea mwamuzi, yeye mwenyewe alikuwa pamoja na mwamuzi yule, akawaokoa toka katika mikono ya waadui zao muda wote wa maisha ya mwamuzi yule. Ingawa hivyo, Yawe aliwaonea huruma aliposikia kilio chao kutokana na mateso na masumbuko yao.
Basi, hasira ya Yawe ikawaka juu ya Israeli, naye akawatia katika mikono ya mufalme wa Mesopotamia, jina lake Kusani, Yule-Mwovu-Sana. Wakamutumikia kwa muda wa miaka minane.