Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 8:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Basi Yesu akawaambia wale Wayuda waliomwamini: “Kama mukitii mafundisho yangu, ninyi ni wanafunzi wangu hakika.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 8:31
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ataokolewa.


Wakati Yesu alipomwona Natanaeli akikuja kwake akasema hivi juu yake: “Angalia Mwisraeli wa kweli asiyekuwa na udanganyifu ndani yake hata kidogo!”


Yesu alialikwa vilevile kwenye ndoa ile pamoja na wanafunzi wake.


Mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli.


Kama Mwana akiwapatia uhuru, basi mutapata uhuru wa kweli.


Nyuma ya mukutano, Wayuda wengi na watu wa mataifa mengine waliogeuka kufuata dini ya Kiyuda, waliomwogopa Mungu, wakawafuata Paulo na Barnaba. Nao wawili wakasema na watu hao na kuwatia moyo kusudi waendelee kutegemea neema ya Mungu.


Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”


Lakini kwa ulinzi wa Mungu ningali muzima hata leo. Nami ninatoa ushuhuda kwa wadogo na wakubwa, wala sisemi maneno mengine yanayokuwa mbali na yale manabii na Musa waliyosema kwamba yatatokea.


Basi ufikiri juu ya wema wa Mungu na ukali wake vilevile. Yeye ni mukali kwa wale walioanguka, lakini yeye ni mwema kwako, ikiwa utaendelea katika wema wake. Kama si vile, wewe vilevile utakatwa.


Wale wanaofanya matendo mema bila kuchoka na kutafuta toka kwa Mungu utukufu, heshima na uzima usiokuwa na mwisho, Mungu atawapa uzima wa milele.


Lakini, inawapasa ninyi kuendelea na musingi imara katika imani, musitikiswe na kupoteza lile tumaini mulilopata wakati muliposikia Habari Njema. Mimi Paulo nimewekwa kuwa mutumishi wa kuhubiri Habari Njema ile iliyokwisha kutangazwa kwa watu wote katika dunia.


Ingawa hivi mwanamuke ataokolewa kwa kuzaa watoto, kama akidumu katika imani, upendo na utakatifu na kuwa mukadirifu.


Ujiangalie wewe mwenyewe na kuangalia mafundisho yako, nawe ushikamane nayo. Kwa maana ukifanya hivi, utajiokoa wewe mwenyewe na kuokoa wale wanaokusikiliza.


Lakini wewe ushikamane na mambo yale uliyofundishwa na kuyaamini kabisa. Unajua ni nani aliyekufundisha.


Kwa maana sisi wote tunaishi katika ushirika na Kristo ikiwa tunachunga mpaka mwisho lile tumaini tulilopata kwa mwanzo.


Agano lile halitakuwa sawa na lile nililofanya na babu zao siku nilipowakamatia kwenye mukono na kuwaondoa toka inchi ya Misri. Kwa sababu hawakushika lile agano, kwa hiyo vilevile sikuwashugulikia. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo.


Lakini mutu anayechunguza sheria kamilifu inayoweka watu huru na kuendelea kushikamana nayo, na si kuisikia tu na kisha kuisahau, lakini anaitimiza kabisa, mutu huyu atabarikiwa na Mungu katika shuguli zake.


Watu hawa wametoka kati yetu, lakini hawakukuwa wa kundi letu, na kwa sababu hii wametuacha. Kama wangekuwa wa kundi letu, wangekaa pamoja nasi. Lakini wametuacha kusudi ionekane wazi ya kama hawakukuwa wa kundi letu.


Kwa hiyo muchunge ndani ya mioyo yenu mafundisho muliyosikia tangia mbele. Kama mukichunga mafundisho yale muliyosikia tangia mbele, mutakaa ndani ya Mwana pamoja na Baba.


Kila mutu atakayeenda mbali na asiyedumu katika mafundisho ya Kristo, mutu yule hashirikiani na Mungu. Lakini yule anayedumu katika mafundisho yale, anashirikiana na Baba na Mwana vilevile.


Kama mukimutii Yawe na kumutumikia na kusikiliza sauti yake bila kuiasi amri yake, kama ninyi wenyewe pamoja na mufalme anayewatawala mukimufuata Yawe, Mungu wenu, basi mutafanikiwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ