Wakati waliposikia maneno haya, wakaondoka wote mumoja kwa mumoja, wakianzia kwa wazee. Yesu akabaki pale peke yake pamoja na yule mwanamuke aliyekuwa akisimama mbele yake.
Basi kama akiolewa na mutu mwingine wakati mume wake angali muzima, atahesabiwa kuwa muzinzi. Lakini kama mume wake akikufa, yeye anakuwa huru toka Sheria ile iliyomufunga na hata akiolewa na mutu mwingine hatahesabiwa kuwa muzinzi.