Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 8:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Ni kwa sababu hii niliwaambia ninyi kama mutakufa katika zambi zenu. Musipoamini kwamba ‘Mimi Ndimi’, hakika mutakufa katika zambi zenu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 8:24
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akamujibu: “Mimi Ndimi Ninayekuwa. Uwaambie watu wa Israeli kwamba: Yule anayeitwa Ndimi Ninayekuwa amekutuma kwao.


Asiyenipata anajizuru mwenyewe; wote wanaonichukia wanapenda kifo.”


Watu wengi watakuja wakijiita kwa jina langu, wakisema: ‘Mimi ni Kristo!’ Nao watawadanganya wengi.


Watu wengi watakuja wakijiita kwa jina langu, wakisema: ‘Mimi ni Kristo!’ Nao watawadanganya wengi.


Anayeamini na kubatizwa ataokolewa, lakini asiyeamini atahukumiwa.


Yesu akawajibu: “Muangalie vizuri, musidanganywe. Watu wengi watakuja wakijiita kwa jina langu, wakisema kwamba wao ndio Kristo, nao wakati umetimia. Ingawa vile, musiwafuate.


Ninawaambia ninyi sasa hayo yote mbele hayajatokea, kusudi wakati yatakapotokea, mwamini kwamba ‘Mimi Ndimi.’


Anayemwamini Mwana hahukumiwi, lakini asiyemwamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakumwamini Mwana wa pekee wa Mungu.


Anayemwamini Mwana yuko na uzima wa milele. Anayekataa kumwamini Mwana hatapata uzima; atakaa akipatwa na kasirani ya Mungu.”


Yesu akamujibu: “Mimi ninayesema nawe, ndiye.”


Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ninajiendea, nanyi mutanitafuta, lakini mutakufa katika zambi zenu. Na zaidi ya hii hamuwezi kufika pahali ninapokwenda.”


Basi wakamwuliza: “Wewe ni nani?” Yesu akawajibu: “Mimi ni yule niliyewaambia tangu mwanzo.


Halafu Yesu akawaambia: “Wakati mutakapomunyanyua Mwana wa Mutu juu, mutafahamu kwamba ‘Mimi Ndimi.’ Na zaidi ya hii mutatambua kwamba sifanyi neno lolote kwa mapenzi yangu, lakini ninasema tu yale niliyofundishwa na Baba.


Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: mbele Abrahamu hajazaliwa, mimi nilikuwa niko.”


“Hivi hakuna anayeweza kuokolewa kwa njia ya mutu mwingine yeyote, kwa maana katika dunia nzima hakuna jina lingine lolote watu walilopewa lenye uwezo wa kuwaokoa.”


Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni?


Basi, namna gani sisi tutaponyoka azabu kama hatushuguliki na wokovu mukubwa kama huu? Ni Bwana mwenyewe aliyetangaza kwanza habari za wokovu huu, na wale waliomusikia walihakikisha kwetu kwamba ni za kweli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ