Yoane 8:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
21 Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ninajiendea, nanyi mutanitafuta, lakini mutakufa katika zambi zenu. Na zaidi ya hii hamuwezi kufika pahali ninapokwenda.”
Ninakuapia kwa jina la Yawe, Mungu wako, Mwenye Uzima, kwamba mufalme amekuwa akikutafuta katika dunia yote. Na mufalme yeyote akisema kwamba haujaonekana kule, Ahabu alimutaka huyo mufalme aape na watu wake kwamba kweli hauko.
Hakutakuwa tena vifo vya watoto wachanga, wazee nao hawatakufa mbele ya wakati wao. Mutu wa miaka mia moja akikufa, amekufa akiwa kijana; na akikufa mbele ya miaka mia moja, ni kusema amelaaniwa.
“Kisha mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kushoto: ‘Muondoke hapa karibu nami, ninyi muliolaaniwa! Muende katika moto usiozimika hata milele, uliotayarishwa kwa ajili ya Shetani na wamalaika wake!
Yesu akawaambia: “Mwangaza ungali kati yenu kwa muda kidogo. Mutembee wakati mungali na mwangaza, kusudi giza lisiwafunike, kwa sababu anayetembea katika giza hajui pahali anapokwenda.
Watoto wangu, ningali pamoja nanyi kwa muda mufupi tu. Mutanitafuta, lakini sawasawa nilivyowaambia Wayuda, ninawaambia ninyi vilevile kwamba hamuwezi kufika pahali ninapokwenda.