Mutu yeyote atakayeua mutu, atahukumiwa kifo kutokana na ushuhuda wa washuhuda wawili au zaidi; mutu yeyote hawezi kuhukumiwa kifo kutokana na ushuhuda wa mutu mumoja.
Lakini kama akikataa kukusikia, utwae mutu mumoja au wawili na kumwendea pamoja nao, kusudi kila neno lihakikishwe kwa ushuhuda wa watu wawili au watatu, sawa vile Maandiko Matakatifu yanavyosema.
Hii ni safari yangu ya tatu ninayotayarisha kuja kwenu. Kama Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Kila neno linapaswa kuhakikishwa kwa ushuhuda wa watu wawili au watatu.”
“Ushuhuda wa mutu mumoja hautoshi kwa kuhukumu mutu juu ya kosa lolote au uovu juu ya kosa lolote alilofanya. Ni ushuhuda wa watu wawili au watatu tu ndio utakaohakishwa.
Nami nitawatuma washuhuda wangu wawili, wakiwa wamevaa nguo za kilio. Nao watatangaza ujumbe wa Mungu kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na makumi sita.”