Mutu yeyote atakayeua mutu, atahukumiwa kifo kutokana na ushuhuda wa washuhuda wawili au zaidi; mutu yeyote hawezi kuhukumiwa kifo kutokana na ushuhuda wa mutu mumoja.
Halafu Paulo akamwambia: “Mungu yeye mwenyewe atakupiga kofi, wewe unayeonekana kwa inje kama ukuta uliopakaliwa chokaa! Wewe unaikaa pale kwa kunihukumu kufuatana na Sheria. Lakini wewe mwenyewe unaivunja kwa kuamuru wanipige!”
Musipendelee mutu yeyote katika kutoa hukumu; mutawasikiliza bila upendeleo, wakubwa kwa wadogo. Musiogopeshwe na sura ya mutu, maana ninyi mutapaswa kuhukumu kwa ajili ya Mungu. Kukikuwa maneno ambayo ni magumu sana kwenu, mutayafikisha kwangu nami nitayasikiliza.’