Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 7:38 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

38 Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: ‘Mito ya maji ya uzima yatatiririka toka ndani ya yule anayeniamini.’ ”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 7:38
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kinywa cha mwenye haki ni chemichemi ya uzima, lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na mateso makali.


Maneno ya kinywa cha mutu ni kilindi cha maji; chemichemi ya hekima ni kijito kinachobubujika.


Mutachota maji kwa furaha kutoka visima vya wokovu.


Viwete watarukaruka kama paa, na bubu wataimba kwa furaha. Maji yatabubujika katika jangwa na vijito katika mbuga.


Nitaimwangilia maji inchi yenye kiu, na kutiririsha muto katika inchi iliyokauka. Nitajaza roho wangu juu ya wazao wako, nitawamwangia watoto wako baraka yangu.


Ee ninyi wote wenye kiu mukuje kwenye maji! Mukuje, wote hata musiokuwa na feza; mununue chakula na mupate kula, mununue divai na maziwa. Bila feza, bila malipo!


Mimi Yawe nitawaongoza siku zote, nitatimiza mahitaji yenu wakati wa shida. Nitawaimarisha katika mwili, nanyi mutakuwa kama bustani iliyomwangiliwa maji, kama chemichemi ya maji ambayo maji yake hayakauki hata kidogo.


Yawe anasema: Mimi ninafanya nanyi agano hili: Roho wangu anayekuwa juu yenu, maneno niliyoyaweka katika kinywa chenu, hayataondoka kwenu hata kidogo, wala kwa watoto na wajukuu wenu, tangu sasa na hata milele.


Wakati ule, maji ya uzima yatabubujika kutoka Yerusalema, na nusu ya maji yale yatatiririkia kwenye bahari ya mashariki, na nusu ingine kwenye bahari ya magaribi. Maji yale yataendelea kububujika wakati wa kipwa kama yanavyokuwa wakati wa mvua.


Yesu akamujibu: “Kama ungejua kitu Mungu anachoweza kukupatia, na ni nani anayekuomba maji ya kunywa, wewe ndiwe ungemwomba, naye angekupa maji ya uzima.”


lakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayomupa, hatasikia kiu tena hata kidogo. Maji nitakayomupa yatakuwa ndani yake kama chemichemi inayotiririka maji ya uzima wa milele.”


kwa maana matunda ya mwangaza ni wema wa kila namna, haki na ukweli.


“Yawe, Mungu wenu atawachagulia nabii anayekuwa kama mimi kutoka kati yenu wenyewe, nanyi mutamutii huyo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ