Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 7:35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

35 Wayuda wakaulizana hivi wao kwa wao: “Mutu huyu atakwenda wapi sisi tusipoweza kumwona? Ataenda kwa Wayuda waliosambazwa kati ya Wagriki na kuwafundisha Wagriki?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 7:35
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe anajenga tena Yerusalema; anawarudisha Waisraeli waliopelekwa katika uhamisho.


Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa kitambulisho kwa mataifa; mataifa yatamutafuta na makao yake yatatukuka.


Naye atasimika bendera kuwaita mataifa, kuwakusanya Waisraeli waliozarauliwa, kuwaleta pamoja watu wa Yuda waliotawanywa, na kuwarudisha toka pembe ine za dunia.


Yeye anasema: Haitoshi tu wewe kuwa mutumishi wangu, kusudi uyainue makabila ya Yakobo, na kurudisha watu wa Israeli waliobaki. Nitakufanya ukuwe mwangaza wa mataifa, kusudi watu wote wapate kuokolewa katika dunia.


–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe, yule anayewakusanya Waisraeli waliosambazwa.– Zaidi ya hao niliokwisha kukusanya, nitawakusanya watu wengine wakutane nao.


Kutoka ngambo ya mito ya Kushi watu wangu wanaoniomba, wale ambao wametawanyika, wataniletea sadaka yangu.


Ndio utakaowaangazia mataifa, na kuleta utukufu kwa watu wako Waisraeli.”


Kulikuwa Wagriki wamoja kati ya wale watu waliofika Yerusalema kuabudu wakati wa sikukuu.


Kisha mambo hayo, Yesu akatembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea katika Yudea, kwa sababu Wayuda walitaka kumwua.


Wakubwa wa Wayuda wakaulizana: “Yeye anasema kwamba hatuwezi kufika pahali anapokwenda; maana yake atakwenda kujiua?”


Wandugu waamini waliposikia maneno hayo, wakatulia na kumusifu Mungu, wakisema: “Kumbe Mungu amewajalia hata watu wa mataifa mengine vilevile kusudi waweze kugeuka toka zambi na kupata uzima kamili.”


Lakini kulitokea wanafunzi wengine, waliokuwa watu wa Kipuro na wa inchi ya Kurene, waliofika Antiokia. Nao wakaanza kusemezana na Wagriki vilevile, wakiwahubiri Habari Njema juu ya Bwana Yesu.


Paulo na Barnaba walipofika katika muji Ikonio, wakaingia vilevile katika nyumba ya kuabudia ya Wayuda. Mule wakahubiri hata kundi kubwa la Wayuda na mataifa mengine wakaamini.


Wamoja kati ya Wayuda wakasadiki na kujiunga pamoja na Paulo na Sila. Vilevile kundi kubwa la Wagriki walioogopa Mungu pamoja na wanawake wengi wenye heshima wakasadiki.


Na kila siku ya Sabato, Paulo alibishana na Wayuda na Wagriki katika nyumba ya kuabudia na kuwashinda.


Lakini wamesikia habari juu yako kwamba unawafundisha Wayuda wote wanaokaa katika inchi za mataifa wasishike Sheria ya Musa. Umewakataza wasiwatahiri watoto wao wala kufuata desturi zetu za kiyuda.


Halafu Bwana akaniambia: ‘Kwenda, kwa maana nitakutuma mbali kwa watu wa mataifa mengine.’ ”


Mimi sisikii haya juu ya Habari Njema, kwa sababu huo ndio uwezo wa Mungu unaowaokoa wote wanaoamini, kwanza Wayuda na kisha watu wa mataifa mengine vilevile.


Mimi ni mudogo kuliko watu wote wa Mungu, lakini Mungu amenijalia neema ya kutangaza kwa watu wa mataifa mengine Habari Njema ya baraka za Kristo zisizoweza kuhesabiwa.


Kwa maana Mungu alitaka kuwafunulia watu hao siri ya mupango wake wenye utajiri mukubwa alioufanya kwa ajili ya mataifa yote. Nayo siri ile ni kwamba Kristo ni ndani yenu, naye ndiye anayetuletea tumaini kwamba tutashiriki katika utukufu wa Mungu.


Ni kwa hiyo nimewekwa kuwa mujumbe na mutume kwa kuwafundisha watu wa mataifa mengine kusudi wapate kumwamini Mungu na kutambua ukweli. Mimi ninasema ukweli wala si uongo.


Kwa ajili ya Habari Njema hii, nimewekwa kuwa mujumbe, mutume na mwalimu,


Barua hii inatoka kwangu mimi Yakobo, mutumishi wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo. Ninawasalimia ninyi watu wa makabila kumi na mawili waliosambazwa katika dunia.


Barua hii inatoka kwangu mimi Petro, mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi muliochaguliwa na Mungu na ambao mulisambazwa, na munaoishi kama wakimbizi kule Ponto, Galatia, Kapadokia, Azia na Bitinia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ