Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 7:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Basi wakatafuta kumufunga, lakini hakuna mutu aliyemukamata, kwa sababu saa yake ilikuwa haijatimia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 7:30
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

wakati ulipoinuka kutimiza hukumu, kuwaokoa wote wanaoteswa katika dunia.


Nilitangaza mambo ya mwisho tangu mwanzo, tangu zamani nilitangaza mambo yatakayotukia. Kusudio langu litatimia; mimi nitatimiza nia yangu yote.


Wafarisayo wakaondoka pale na kwenda kufanya shauri la kumwua Yesu.


Kwa hiyo wakatafuta kumukamata, lakini waliogopa makundi ya watu kwa sababu wao walisadiki kwamba yeye ni nabii.


Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria walipopata habari hii, wakatafuta njia ya kumwua Yesu. Lakini walimwogopa, kwa sababu kundi lote la watu walishangaa na mafundisho yake.


Saa ile ile wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria wakatafuta kumukamata, kwa sababu walitambua kwamba alisema mufano huo juu yao.


Siku zote nilipokuwa pamoja nanyi katika hekalu, ninyi hamukunikamata. Lakini hii ni saa yenu; saa ya utawala wa bwana wa giza.”


Halafu Wayuda wakaokota tena mawe kwa kumutupia.


Wakajaribu tena kumufunga Yesu, lakini akawaponyoka.


Nao wakubwa wa makuhani na Wafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mutu akijua pahali Yesu alipokuwa, alete habari kusudi wapate kumufunga.


Musa hakuwapa ninyi Sheria? Ingawa hivyo hakuna mumoja wenu anayetii Sheria. Na sasa sababu gani munatafuta kuniua?”


Wafarisayo wakasikia maneno hayo watu waliyosemasema juu ya Yesu. Basi wakubwa wa makuhani na Wafarisayo wakatuma walinzi wao kumufunga.


Na Yesu akawaambia: “Wakati unaofaa kwangu haujatimia; lakini wakati wowote unafaa kwenu.


Ninyi muende kwa sikukuu. Mimi sijaenda bado kwa sikukuu hii, kwa sababu wakati unaofaa kwangu haujatimia.”


Yesu alisema maneno haya wakati alipokuwa akifundisha katika hekalu, kwenye sanduku za kuwekea matoleo. Hakuna mutu aliyemufunga, kwa sababu wakati wake ulikuwa haujatimia.


Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Abrahamu. Lakini munatafuta kuniua, kwa sababu munakataa kukubali mafundisho yangu.


Kwa ajili ya hii, wakaokota mawe kwa kumutupia. Lakini Yesu akajificha na kutoka ndani ya hekalu.


Imetupasa kufanya kazi za yule aliyenituma wakati kungali muchana, kwa sababu usiku unakaribia, wakati mutu asipoweza kutumika.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ