24 Muache kuhukumu kufuatana na hali ya inje, lakini muhukumu kwa haki.”
“Mpaka wakati gani mutaendelea kuhukumu bila haki na kuwapendelea watu waovu?
Kumuhesabu mwovu kuwa na haki na kumwazibu asiyekuwa na kosa, yote mawili ni chukizo kwa Yawe.
Hii ni misemo mingine ya wenye hekima. Kupendelea watu katika hukumu si vizuri.
Kwa ajili ya kituliro kidogo wanawaachilia wenye kosa na kuwanyima wasiokuwa na kosa haki yao.
Unapotoa hukumu uamue kwa haki, usimupendelee masikini wala kumwogopa mwenye cheo. Lakini hukumu mwenzako kwa haki.
Yawe wa majeshi anasema hivi: Mutoe hukumu kwa haki, mutende mema na kuwa na huruma ninyi kwa ninyi.
Halafu watu wamoja wa Yerusalema wakasema: “Huyu si mutu yule wanayetafuta kumwua?
Ninyi munahukumu kwa kufuatana na mafikiri ya kimutu; lakini mimi simuhukumu mutu.
Ninyi munaangalia tu namna vitu vinavyoonekana kwa inje. Mutu yeyote anayejiaminia kwamba yeye ni wa Kristo, inafaa afikiri tena yeye mwenyewe mambo haya: ikiwa yeye ni wa Kristo sisi vilevile ni wa Kristo.
Wandugu zangu, kufuatana na vile munavyomwamini Bwana wetu Yesu Kristo mwenye utukufu, musikuwe vilevile na upendeleo na watu.
Jambo hilo halionyeshi kwamba munafanya ubaguzi, na kwamba kwa kuamua vile munaongozwa na mawazo mabaya?
Lakini kama mukifanya upendeleo, munafanya zambi, nanyi munahukumiwa na Sheria kwa sababu mumeivunja.