Yoane 7:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
23 Basi, kama munaweza kutahiri mutu kwa siku ya Sabato, kusudi musivunje Sheria ya Musa, kwa nini munanikasirikia kwa sababu nimemuponyesha mutu kabisa kwa siku ya Sabato?
Mutashika Sabato, nayo itakuwa kwenu siku takatifu. Yeyote atakayeichafua siku hiyo anapaswa kuuawa. Na mutu atakayefanya kazi yoyote siku hiyo atatengwa mbali na watu wake.
Mule ndani mulikuwa mutu mumoja mwenye mukono unaokauka. Nao watu wamoja waliokuwa pale walitafuta sababu ya kumushitaki Yesu; kwa hiyo wakamwuliza: “Sheria yetu inaruhusu kumuponyesha mutu kwa siku ya Sabato?”
Vilevile hamujasoma bado katika kitabu cha Sheria ya Musa kwamba kila siku ya Sabato, makuhani wanaotumika ndani ya hekalu wanavunja Sheria inayoelekea siku ile, nao hawahesabiwi kuwa na kosa?
Wafarisayo wamoja wakasema: “Mutu huyu hakutoka kwa Mungu kwa sababu hashiki sheria ya siku ya Sabato.” Lakini wengine wakasema: “Mutu mwenye zambi anaweza kuonyesha kitambulisho kama hiki?” Basi kukatokea mikorogano kati yao.