Hauamini kwamba mimi na baba ni mumoja, yeye ni ndani yangu na mimi ndani yake? Maneno ninayowaambia siyasemi kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini Baba anayekaa ndani yangu ndiye anayefanya kazi zake.
“Siwezi kufanya kitu kwa mafikiri yangu mwenyewe. Ninahukumu tu kama vile Mungu anavyoniambia na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu sitafuti kufanya mapenzi yangu, lakini mapenzi ya yule aliyenituma.
Halafu Yesu akawaambia: “Wakati mutakapomunyanyua Mwana wa Mutu juu, mutafahamu kwamba ‘Mimi Ndimi.’ Na zaidi ya hii mutatambua kwamba sifanyi neno lolote kwa mapenzi yangu, lakini ninasema tu yale niliyofundishwa na Baba.
Kila mutu atakayeenda mbali na asiyedumu katika mafundisho ya Kristo, mutu yule hashirikiani na Mungu. Lakini yule anayedumu katika mafundisho yale, anashirikiana na Baba na Mwana vilevile.
Hizi ni habari za mambo yaliyofunuliwa na Yesu Kristo. Kristo alipata ufunuo huu kutoka kwa Mungu, kusudi awaonyeshe watumishi wake mambo yanayopaswa kutokea kisha kidogo. Kristo alimutuma malaika wake kwa kumujulisha mutumishi wake Yoane mambo yale.