Yoane 7:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
12 Katika kundi lile kulikuwa manunguniko mengi juu yake. Wamoja walisema: “Yeye ni mutu muzuri.” Wengine walisema: “Hapana, si vile, yeye anawadanganya watu.”
Lakini inatosha kwa mwanafunzi kufanana na mwalimu wake na mutumishi kufanana na bwana wake. Ikiwa wanamwita mukubwa wa jamaa Belzebuli, hawatakosa kuwaita watu wa jamaa yake kwa majina mabaya zaidi.
Kulikuwa mutu mumoja muzaliwa wa Arimatea, katika jimbo la Yuda, jina lake lilikuwa Yosefu. Mutu huyu alikuwa mwema na mwenye haki, naye alikuwa akitazamia Ufalme wa Mungu. Yeye alikuwa mumoja wa washauri wa Baraza Kubwa, lakini hakukubali shauri na matendo ya wenzake.
Mutu muzuri anasema maneno mazuri kutokana na uzuri wa moyo wake. Na mutu mubaya anasema maneno mabaya kutokana na ubaya wa moyo wake. Kwa maana kinywa cha mutu kinasema maneno yanayojaa ndani ya moyo wake.
Wafarisayo wamoja wakasema: “Mutu huyu hakutoka kwa Mungu kwa sababu hashiki sheria ya siku ya Sabato.” Lakini wengine wakasema: “Mutu mwenye zambi anaweza kuonyesha kitambulisho kama hiki?” Basi kukatokea mikorogano kati yao.