11 Wayuda walikuwa wakimutafuta kwenye sikukuu ile na kuuliza kwamba yeye yuko wapi.
Huu ndio ushuhuda wa Yoane kwa makuhani na Walawi waliotumwa na Wayuda kutoka Yerusalema kumwuliza kwamba yeye ni nani.
Wakamutafuta Yesu, na wakaulizana hivi ndani ya hekalu: “Munawaza nini? Atakuja kwa karamu au hapana?”
Kisha mambo hayo, Yesu akatembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea katika Yudea, kwa sababu Wayuda walitaka kumwua.
Lakini hakuna mutu aliyesema juu yake waziwazi, kwa sababu waliwaogopa wakubwa wa Wayuda.
Wayuda wakashangaa, wakisema: “Mutu huyu amepata elimu kama hii namna gani, naye hakufundishwa?”
Nao wakamwuliza tena: “Yule mutu yuko wapi?” Akajibu: “Sijui.”