Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 6:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 “Hapa kuna mutoto mumoja anayekuwa na mikate mitano ya shayiri pamoja na samaki mbili. Lakini chakula hiki hakitawafalia kitu watu wengi kama hawa.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 6:9
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Elisha akamujibu: “Sikiliza neno la Yawe: Kesho kwa wakati kama huu, humu Samaria kilo tatu za unga bora wa ngano zitanunuliwa kwa kipande kimoja cha feza, na kilo sita za shayiri kwa kipande kimoja cha feza.”


Analeta amani katika eneo lako; anakushibisha kwa ngano safi kabisa.


Walimutukana Mungu wakisema: “Hakika, Mungu anaweza kutupatia chakula katika jangwa?


Walimujaribu Mungu tena na tena, wakamukasirikisha huyo Mutakatifu wa Israeli.


Wanaonichukia wangenipigia magoti kwa hofu, na azabu yao ingekuwa ya milele.


Hata watu wa inchi ya Yuda na ya Israeli walifanya biashara nawe; walikupa ngano, mizeituni, tini za kwanzakwanza, asali, mafuta na marasi kwa kununua vitu kwako.


Lakini wao wakamujibu: “Hapa tuko tu na mikate mitano na samaki mbili.”


Hamujaelewa bado? Hamukumbuki ile mikate mitano niliyoshibisha nayo watu elfu tano, nayo ile hesabu ya vitunga mulivyojaza?


Naye Yesu akawauliza: “Muko na mikate ngapi? Muende kwanza kuangalia.” Walipokwisha kujua, wakamwambia: “Tuko na mikate mitano na samaki mbili.”


wakati nilipomega mikate mitano na kulisha watu elfu tano? Wakati ule mulijaza vitunga ngapi na vipande vya mikate?” Wakajibu: “Kumi na viwili.”


Lakini Yesu akawajibu: “Ninyi wenyewe muwape chakula!” Nao wakajibu: “Sisi tuko tu na mikate mitano na samaki mbili. Unataka sisi wenyewe tuende kuwanunulia watu hawa wote chakula?”


Marta akamwambia Yesu: “Bwana, kama ungekuwa hapa, kaka yangu hangekufa.


Maria alipofika pale Yesu alipokuwa na kumwona, akaanguka kwenye miguu yake na kusema: “Bwana, kama ungekuwa hapa, kaka yangu hangekufa.”


Yesu akawaambia: “Mulete sehemu ya samaki munaotoka kuvua.”


Basi Yesu akawajongelea, akatwaa mukate, akawagawanyia; na kuwapa samaki vilevile.


Walipofika inchi kavu wakaona mukate na samaki zinazokuwa juu ya moto.


Kisha Yesu akatwaa ile mikate, akamushukuru Mungu na kuigawanya kwa watu walioikaa pale. Akawapa samaki vilevile kwa kadiri walivyotaka.


Filipo akamujibu: “Hata tukinunua mikate kwa bei ya vikoroti mia mbili vya feza, haitatosha kwa kumupa kila mutu hata kidogo tu.”


Kwa maana munajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, ingawa alikuwa tajiri, yeye mwenyewe alijifanya masikini kwa ajili yenu, kusudi mupate kuwa watajiri kwa njia ya umasikini wake.


Aliwapa siagi na maziwa ya mifugo, mafuta ya wana-kondoo na kondoo dume, makundi ya mifugo ya Basani na mbuzi. Aliwapa ngano nzuri kabisa na divai mupya wakakunywa.


inchi yenye ngano na shayiri, mizabibu, mitini, mikomamanga, mizeituni na asali.


Nikasikia kitu kama sauti iliyotokea katikati ya vile viumbe vine vya ajabu ikisema: “Kilo moja ya ngano ni mushahara wa siku nzima ya kazi, na kilo tatu ya shayiri ni mushahara wa siku nzima ya kazi, lakini usiharibu mafuta wala divai.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ