Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 6:51 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

51 Mimi ni ule mukate wa uzima, ulioshuka toka mbinguni. Kama mutu akikula mukate huu ataishi milele. Na mukate nitakaotoa ni mwili wangu, utakaotolewa kusudi dunia ipate uzima.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 6:51
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa maana Mwana wa Mutu hakukuja kutumikiwa, lakini kutumikiana na kutoa maisha yake kusudi awakomboe watu wengi.”


Halafu akatwaa mukate, akaubariki, kisha akaumega na kuwapa akisema: “Huu ni mwili wangu [unaotolewa kwa ajili yenu. Mufanye hivi kwa kunikumbuka.”


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Vilevile yeyote anayeishi ndani yangu na kuniamini, hatakufa hata milele. Unaamini maneno haya?”


Na zaidi ya hii hakuna mutu aliyepanda mbinguni, isipokuwa Mwana wa Mutu aliyeshuka toka mbinguni.


Sawa Musa alivyonyanyua nyoka ya shaba juu ya muti katika jangwa, ni hivi vilevile, sherti Mwana wa Mutu anyanyuliwe,


Kwa maana Mungu alipenda sana ulimwengu hata kumutoa Mwana wake wa pekee, kusudi kila mutu anayemwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.


Anayemwamini Mwana yuko na uzima wa milele. Anayekataa kumwamini Mwana hatapata uzima; atakaa akipatwa na kasirani ya Mungu.”


“Kweli, kweli ninawaambia: anayesikia neno langu na kumwamini yule aliyenituma, anapata uzima wa milele. Yeye hatahukumiwa, lakini ameponyoka lufu na kupata uzima.


Maana mukate Mungu anaoupana ni yule anayeshuka toka mbinguni na kuleta uzima katika dunia.”


Yesu akawaambia: “Mimi ni mukate wa uzima. Anayenikubali hatasikia njaa hata kidogo, na yule anayeniamini hatasikia kiu hata kidogo.


Basi Wayuda wakaanza kunungunika kwa sababu Yesu alisema kwamba yeye ni mukate ulioshuka toka mbinguni.


Kweli, kweli ninawaambia: anayeamini anapata uzima wa milele.


Lakini ule ni mukate ulioshuka toka mbinguni, anayeukula hatakufa.


Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: ‘Mito ya maji ya uzima yatatiririka toka ndani ya yule anayeniamini.’ ”


Ndiyo kusema, Mungu ndiye aliyekuwa akipatanisha watu wote na yeye mwenyewe kwa njia ya Kristo bila kuhesabu makosa yao. Yeye ametupatia ujumbe wa upatanisho.


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.


Nanyi waume muwapende wake wenu sawa vile Kristo alivyopenda kanisa na kutoa uzima wake kwa ajili yake.


Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu, kusudi atukomboe toka uovu wote na kututakasa tupate kuwa watu wake wa pekee, watu wanaokuwa na hamu ya kufanya kazi nzuri.


Yeye ametufungulia njia mupya ya uzima, inayopitia katika pazia, maana yake mwili wake mwenyewe.


Mumwendee Bwana. Yeye ni jiwe lenye uzima. Jiwe lile lilitupiliwa na watu lakini lilichaguliwa na Mungu, nalo linahesabiwa kuwa la bei kali mbele yake.


Yeye ndiye sadaka iliyotolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu, wala si kwa ajili ya zambi zetu tu, lakini kwa ajili ya zambi za watu wote.


Na huu ndio upendo: si kwamba sisi tulimupenda Mungu, lakini kwamba ni yeye ndiye aliyetupenda hata akatuma Mwana wake kama vile sadaka iliyotolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu.


Na sisi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemutuma Mwana wake kuwa Mwokozi wa dunia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ