Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 6:39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

39 Na mapenzi ya yule aliyenituma ni kwamba nisipoteze hata mumoja wa wale alionipa, lakini nimufufue siku ya mwisho wa dunia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 6:39
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitawapa wachungaji watakaowatunza vema, nao hawatakuwa na woga tena wala kufazaika, na hakuna hata mumoja wao atakayepotea. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kweli ninawaambia: kwa Siku ya hukumu, watu wa muji ule wataazibiwa vikali zaidi kuliko watu wa muji wa Sodoma na wa Gomora.


Ni hivi vilevile Baba yenu anayekuwa mbinguni hataki hata mumoja wa hawa wadogo kupotea.


“Musiogope ninyi kundi dogo! Kwa kuwa Baba yenu amependelea kuwapa ninyi ule Ufalme wake.


Yule anayenikataa na asiyekubali maneno yangu atahukumiwa kufuatana nayo. Ni lile neno nililosema ndilo litakalomuhukumu siku ya mwisho.


Wakati nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda kwa uwezo wa jina lako, ndilo lile jina ulilonipa. Nimewachunga wala hakuna mumoja wao aliyepotea, isipokuwa yule anayepaswa kupotea, kusudi Maandiko Matakatifu yatimizwe.


Kwa maana ulimupa mamlaka juu ya watu wote, kusudi awapatie uzima wa milele wale wote uliomupa.


“Baba, ninataka wale ulionipa wakuwe pamoja nami pahali nitakapokuwa, nao waone utukufu wangu, ndio ule utukufu ulionipa kwa sababu ulinipenda mbele ya kuumbwa kwa dunia.


“Nimekujulisha kwa watu wale ulionipa, ukiwachagua katika dunia. Wao walikuwa watu wako, uliwatoa kwangu, nao walishika neno lako.


“Ninawaombea wao; siwaombei watu wa dunia, lakini hao ulionipa, kwa sababu wao ni wako.


Alisema vile kusudi maneno haya aliyosema yapate kutimia: “Sikupoteza hata mumoja kati ya wale ulionipa.”


Musishangae kwa ajili ya maneno haya, kwa sababu kutakuwa wakati wafu wote wanaokuwa ndani ya makaburi watakaposikia sauti yake


Wote Baba anaonipa wanakuja kwangu; nami sitamukataa hata kidogo yule anayekuja kwangu.


Hakika mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mutu anayemwona Mwana na kumwamini apate uzima wa milele, nami nitamufufua siku ya mwisho.”


Hakuna mutu anayeweza kuja kwangu, isipokuwa anavutwa na Baba aliyenituma, nami nitamufufua siku ya mwisho.


Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anapata uzima wa milele, nami nitamufufua siku ya mwisho.


Na kama Roho wa Mungu aliyemufufua Yesu anakaa ndani yenu, basi huyo aliyemufufua Kristo ataupatia mwili wenu unaokuwa wa kufa uzima kwa njia ya Roho wake anayekaa ndani yenu.


Mungu aliyemufufua Bwana Yesu atatufufua nasi vilevile kwa uwezo wake.


Lakini musingi uliojengwa na Mungu, unasimama imara. Nayo maneno haya yamechapwa juu ya musingi ule “Bwana anajua wale wanaokuwa wake,” na haya mengine: “Kila mutu anayesema kwamba yeye ni wa Bwana anapaswa kujitenga na maovu.”


Nao wakiomba kwa imani, mugonjwa yule atapona, kwa kuwa Bwana atamurudishia afya yake. Na ikiwa amefanya zambi, atasamehewa.


Ninyi ambao kwa imani munalindwa salama kwa nguvu za Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa kwa mwisho wa nyakati.


Barua hii inatoka kwangu mimi Yuda, mutumishi wa Yesu Kristo na ndugu wa Yakobo. Ninawaandikia ninyi mulioitwa na Mungu Baba na munaoishi katika upendo wake na kulindwa kwa ajili ya Yesu Kristo.


Kukitokea watu wanaokufuatilia na kutaka kuyaangamiza maisha yako, Yawe, Mungu wako, atayalinda maisha yako pamoja na watu wanaokuwa wazima. Lakini atayatupilia mbali maisha ya waadui zako, kama vile mutu anavyotupa jiwe kwa mujeledi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ