Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 6:37 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

37 Wote Baba anaonipa wanakuja kwangu; nami sitamukataa hata kidogo yule anayekuja kwangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 6:37
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe atajenga upya Sayuni, na kuonyesha utukufu wake.


Watu wako watajitolea, siku utakapokwenda kuwapiga waadui. Juu ya milima mitakatifu vijana wako watakufikia, kama umande unaotokeza asubui mapema.


wewe niliyekuleta toka miisho ya dunia, niliyekuita toka mbali kwa mipaka ya dunia, wewe niliyekuambia: Wewe ni mutumishi wangu; mimi sikukutupilia, lakini nilikuchagua.


Hatavunja tete lililokunjama, hatazimisha utambi unaotoa moshi; ataimarisha sheria yangu kwa uaminifu.


Waovu waache njia zao mbaya, watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya; wamurudilie Yawe apate kuwahurumia, wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.


“Mukuje kwangu ninyi wote munaosumbuka na kulemewa na mizigo mizito, nami nitawapumzisha.


kwa maana kutatokea watu wanaojiita kwa uongo ‘Kristo’ pamoja na manabii wa uongo, nao wataonyesha vitambulisho vikubwa na maajabu, hata ikiwezekana, wawadanganye hata watu waliochaguliwa na Mungu.


Mimi sitabaki tena katika dunia, lakini wao wangali katika dunia na mimi ninakuja kwako. Baba Mutakatifu, uwalinde kwa uwezo wa jina lako, lile jina ulilonipa, kusudi wakuwe mumoja kama vile sisi tunavyokuwa mumoja.


Kwa maana ulimupa mamlaka juu ya watu wote, kusudi awapatie uzima wa milele wale wote uliomupa.


“Baba, ninataka wale ulionipa wakuwe pamoja nami pahali nitakapokuwa, nao waone utukufu wangu, ndio ule utukufu ulionipa kwa sababu ulinipenda mbele ya kuumbwa kwa dunia.


“Nimekujulisha kwa watu wale ulionipa, ukiwachagua katika dunia. Wao walikuwa watu wako, uliwatoa kwangu, nao walishika neno lako.


Na mapenzi ya yule aliyenituma ni kwamba nisipoteze hata mumoja wa wale alionipa, lakini nimufufue siku ya mwisho wa dunia.


Yesu akaongeza kusema: “Kwa sababu hii niliwaambia kama hakuna mutu anayeweza kuja kwangu, isipokuwa anawezeshwa na Baba.”


Wakamujibu: “Wewe, uko mwenye zambi kabisa tangu kuzaliwa kwako! Unataka kutufundisha?” Halafu wakamufukuza inje.


Sheria ilitokea na kusababisha kuongezeka kwa makosa, lakini nafasi yoyote palipozidi zambi, neema ilizidi sana.


Kwa maana Mungu amewapa ninyi neema ya kumutumikia Kristo, na si kwa kumwamini tu, lakini vilevile kwa kuteswa kwa ajili yake.


lakini kwa sababu hiyo Mungu amenihurumia. Alifanya vile kusudi kwa njia yangu mimi ninayekuwa mutenda zambi wa kwanza, Yesu Kristo apate kuonyesha uvumilivu wake. Na hivi mimi nipate kuwa mufano kwa wote watakaoamini nyuma na kupata uzima wa milele.


Lakini musingi uliojengwa na Mungu, unasimama imara. Nayo maneno haya yamechapwa juu ya musingi ule “Bwana anajua wale wanaokuwa wake,” na haya mengine: “Kila mutu anayesema kwamba yeye ni wa Bwana anapaswa kujitenga na maovu.”


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.


Watu hawa wametoka kati yetu, lakini hawakukuwa wa kundi letu, na kwa sababu hii wametuacha. Kama wangekuwa wa kundi letu, wangekaa pamoja nasi. Lakini wametuacha kusudi ionekane wazi ya kama hawakukuwa wa kundi letu.


Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ