Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 6:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Wakamwuliza: “Basi utatuonyesha kitambulisho gani kusudi tupate kukiona na kukuamini? Utafanya jambo gani?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 6:30
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutu huyo akaonyesha kitambulisho siku ileile, akasema: “Hiki ndicho kitambulisho Yawe alichosema: ‘Mazabahu hii itabomoka, na majivu yanayokuwa juu yake yatamwangika.’ ”


Mazabahu nayo ikabomoka, na majivu yake yakamwangika chini, kama kitambulisho kile yule mutu wa Mungu alichokitoa na ujumbe wa Yawe.


Mungu akamwambia Musa: “Wasipokuamini au kusadiki kitambulisho cha kwanza, inawezekana wataamini kitambulisho cha pili.


“Mufalme wa Misri atakapowaambia muhakikishe jambo lile kwa kutenda miujiza, wewe utamwambia Haruni atwae fimbo yake, aitupe mbele ya mufalme, nayo itakuwa nyoka.”


Wanasema: Muache Yawe afanye haraka, tunataka kuona yale aliyosema atayafanya! Mutakatifu wa Israeli atimize basi kusudi lake kusudi tuone ana mipango gani!


Kristo, Mufalme wa Waisraeli, ajishushe sasa juu ya musalaba, kusudi nasi tupate kuona na kumwamini.” Hata wale waliotundikwa pamoja naye walimutukana vilevile.


Wafarisayo wakamufikia Yesu na kuanza kubishana naye. Wakamupima wakimwomba awaonyeshe kitambulisho kinachohakikisha kwamba uwezo wake umetoka kwa Mungu.


Lakini kama nikiyatenda, hata ikiwa hamuniamini mimi, basi mwamini matendo yangu, kusudi mupate kujua kabisa kwamba mimi na Baba ni mumoja, yeye ni ndani yangu, nami ndani yake.”


Ingawa vitambulisho vyote alivyoonyesha mbele yao, hawakumwamini,


Basi Wayuda wakamwuliza: “Utaonyesha kitambulisho gani kwa kutuhakikishia kwamba uko na haki ya kufanya hivi?”


(Wakati ule wanafunzi wake walikuwa wamekwenda katika muji kununua vyakula.)


Watu walipoona kile kitambulisho Yesu alichoonyesha, wakasema: “Hakika mutu huyu ndiye yule nabii aliyepaswa kuja katika dunia!”


Kundi kubwa la watu wakamufuata, kwa sababu watu hao waliona vitambulisho alivyoonyesha kwa kuponyesha wagonjwa.


Lakini kama nilivyowaambia: mumeniona, lakini ijapokuwa vile hamuamini.


Utumie nguvu zako kwa kuponyesha watu, kwa kufanya maajabu na vitambulisho kwa uwezo wa jina la mutumishi wako mutakatifu Yesu.”


Wayuda wanaomba kuonyeshwa vitambulisho nao Wagriki wanatafuta hekima.


Mungu vilevile alihakikisha ushuhuda wao kwa njia ya maajabu, ya miujiza mbalimbali, na ya vitambulisho, na kwa njia ya zawadi za Roho Mutakatifu alizowapa watu kama anavyopenda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ