29 Yesu akawajibu: “Hii ndiyo kazi ya Mungu: mumwamini yule aliyemutuma.”
Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”
Anayeamini na kubatizwa ataokolewa, lakini asiyeamini atahukumiwa.
Anayemwamini Mwana yuko na uzima wa milele. Anayekataa kumwamini Mwana hatapata uzima; atakaa akipatwa na kasirani ya Mungu.”
Munachunguza Maandiko Matakatifu, kwa maana munazani kuwa ndani yao mutapata uzima wa milele. Maandiko hayo ndiyo yanayonishuhudia,
Basi wakamwuliza: “Tufanye nini kusudi tupate kutumika kazi ya Mungu?”
Kwa sababu nimeshuka toka mbinguni kusudi nifanye mapenzi ya yule aliyenituma, wala si mapenzi yangu.
Kama vile Baba aliyenituma anavyokuwa muzima, nami ninaishi kwa nguvu zake, vilevile anayenikula ataishi kwa nguvu zangu.
Nao wakajibu: “Umwamini Bwana Yesu, nawe utaokolewa pamoja na watu wote wa nyumba yako.”
Kwa maana tunakumbuka mbele ya Mungu Baba yetu namna munavyotumika kwa imani na munavyojisumbua na kazi kwa ajili ya upendo wenu. Vilevile tunakumbuka namna tumaini lenu katika Yesu Kristo linavyokuwa imara.
Na alipokwisha kufanywa kuwa mukamilifu, akawaongoza watu wote wanaomutii wapate kuokolewa kwa milele.
Basi unaona kwamba imani yake ilionekana kwa njia ya matendo yake na kwa njia hiyo ikapata kukamilishwa.
Amri yake ndiyo hii tuamini jina la Mwana wake Yesu Kristo na tupendane sisi kwa sisi kama vile Kristo alivyotuamuru.
Mutu yeyote anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo, yeye ni mutoto wa Mungu; na kila mutu anayemupenda baba anamupenda mwana wake vilevile.
Na yule atakayeshinda na kuendelea kufuata mapenzi yangu mpaka mwisho, nitamupa mamlaka ya kutawala mataifa.