Sasa, mwanamuke huyu anayekuwa wa uzao wa Abrahamu, ambaye alifungwa na Shetani kwa muda wa miaka kumi na minane, haikumupasa afunguliwe katika kifungo hiki ingawa ni siku ya Sabato?”
Kati yao kulikuwa mwanamuke mumoja mwenye ugonjwa wa kutokwa na damu kwa muda wa miaka kumi na miwili. Alikuwa ametumia mali yake yote kwa kulipa waganga, lakini hakuna hata mumoja wao ambaye aliweza kumuponyesha.
kwa sababu malaika wa Bwana alishuka mara kwa mara ndani ya kile kisima na kutikisa maji. Na mugonjwa wa kwanza aliyeingia ndani ya maji kisha kuyatikisa, alipona ugonjwa wowote aliokuwa nao.]
Lakini hatujui kilichotokea hata anaona sasa, wala hatujui ni nani aliyemuponyesha macho. Yeye ni mutu muzima. Mumwulize yeye mwenyewe, naye atawaelezea maneno yake.”
Karibu na mulango mumoja wa hekalu unaoitwa “Muzuri,” kulikuwa mutu mumoja aliyekuwa kiwete tangia kuzaliwa kwake. Kila siku walimubeba na kumuweka kwenye mulango huo kusudi aombe musaada kwa watu waliokuwa wakiingia katika hekalu.