Wazao wako watakuwa wengi kama mavumbi ya dunia, na urizi wao utaenea kila pahali: upande wa magaribi, mashariki, kaskazini na kusini. Kwa njia yako na ya wazao wako, jamaa zote katika dunia zitabarikiwa.
Kisha akawaelezea maneno yaliyoandikwa juu yake katika Maandiko Matakatifu yote, akianza toka vitabu vya Musa na kuendelea katika vitabu vya manabii wote.
Kisha Filipo akamukuta Natanaeli, akamwambia: “Tumemwona yule ambaye Musa aliandika habari zake katika kitabu cha Sheria na ambaye manabii walisema juu yake. Ni Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”
Lakini kwa ulinzi wa Mungu ningali muzima hata leo. Nami ninatoa ushuhuda kwa wadogo na wakubwa, wala sisemi maneno mengine yanayokuwa mbali na yale manabii na Musa waliyosema kwamba yatatokea.
Maana kufuatana na Sheria hiyo, mimi nimekuwa kama mufu, na kifo kile kimesababishwa na Sheria. Imetokea vile kusudi nipate kuishi kwa ajili ya Mungu. Mimi nimekufa pamoja na Kristo juu ya musalaba.
Lakini wale wanaotegemea kutimiza yale yanayoamuriwa na Sheria, wamelaaniwa. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Alaaniwe mutu yeyote asiyedumu katika yote yanayoandikwa katika hiki kitabu cha Sheria na kuyatii.”
Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”