Wakati waliposikia maneno haya, wakaondoka wote mumoja kwa mumoja, wakianzia kwa wazee. Yesu akabaki pale peke yake pamoja na yule mwanamuke aliyekuwa akisimama mbele yake.
Wote wanaofanya zambi pasipo kujua Sheria ya Musa watapotea pasipo kuhukumiwa na Sheria ile. Lakini wote wanaofanya zambi wakijua Sheria watahukumiwa kufuatana na Sheria.
Lakini wale wanaotegemea kutimiza yale yanayoamuriwa na Sheria, wamelaaniwa. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Alaaniwe mutu yeyote asiyedumu katika yote yanayoandikwa katika hiki kitabu cha Sheria na kuyatii.”