Lakini Abisayi mwana wa Zeruya alikwenda kumusaidia Daudi. Abisayi alimushambulia yule Mufilistini na kumwua. Kwa hiyo, watu wakamwapia Daudi wakisema: “Hautakwenda tena nasi katika vita, kusudi usiizime taa ya ufalme katika Israeli.”
Basi, wanakuja kwako makundi kwa makundi na kuikaa mbele yako kama watu wangu, kusudi wasikie unachosema, lakini hawafanyi unachowaambia wafanye. Wanasema kwamba wana upendo, lakini hayo ni kusema tu; wanachotafuta kwa moyo ni faida yao tu.
“Kweli ninawaambia: kati ya watu wanaoishi katika dunia, hakuna mutu anayekuwa mukubwa kuliko Yoane Mubatizaji. Lakini yeyote anayeonekana kuwa mudogo katika Ufalme wa mbinguni anahesabiwa kuwa mukubwa kuliko yeye.
Lakini vilevile kwa kuwa tunaogopa watu hawa, hatuwezi kusema kwamba yalitoka kwa mutu; kwa maana watu hawa wote wanasadiki kwamba Yoane alikuwa nabii.”
Herode alimwogopa Yoane, kwa sababu alijua kwamba Yoane ni mwenye haki na mutakatifu. Kwa hivi alimulinda. Alipenda kumusikiliza, ijapokuwa alifazaika sana kila mara alipomusikia.
Ninawaambia: kati ya watu wanaoishi katika dunia, hakuna anayekuwa mukubwa kuliko Yoane. Lakini yeyote anayehesabiwa kuwa mudogo katika Ufalme wa Mungu anahesabiwa kuwa mukubwa kuliko yeye.”
Vilevile tunaamini ujumbe uliotangazwa na manabii. Ninyi munafanya vema mukishikamana nao. Ujumbe huo ni kama taa inayoangaza pahali pa giza, mpaka wakati wa mapambazuko na wakati nyota ya asubui itakapoangazia mioyo yenu.