Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 5:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 “Kweli, kweli ninawaambia: anayesikia neno langu na kumwamini yule aliyenituma, anapata uzima wa milele. Yeye hatahukumiwa, lakini ameponyoka lufu na kupata uzima.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 5:24
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu hawa watakwenda kwenye nafasi watakapoazibiwa kwa milele, lakini wenye haki wataingia kwenye uzima wa milele.”


Anayeamini na kubatizwa ataokolewa, lakini asiyeamini atahukumiwa.


Vilevile yeyote anayeishi ndani yangu na kuniamini, hatakufa hata milele. Unaamini maneno haya?”


Halafu Yesu akasema hivi kwa sauti: “Anayeniamini haniamini mimi tu, lakini anamwamini vilevile yule aliyenituma.


Lakini hii imeandikwa kusudi mupate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mupate uzima katika jina lake.


Kwa maana Mungu alipenda sana ulimwengu hata kumutoa Mwana wake wa pekee, kusudi kila mutu anayemwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.


Anayemwamini Mwana hahukumiwi, lakini asiyemwamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakumwamini Mwana wa pekee wa Mungu.


Anayemwamini Mwana yuko na uzima wa milele. Anayekataa kumwamini Mwana hatapata uzima; atakaa akipatwa na kasirani ya Mungu.”


Muvunaji anakwisha kupokea mushahara, naye anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele, kusudi mupandaji na muvunaji wafurahi pamoja.


Hakika mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mutu anayemwona Mwana na kumwamini apate uzima wa milele, nami nitamufufua siku ya mwisho.”


Kweli, kweli ninawaambia: anayeamini anapata uzima wa milele.


Lakini ule ni mukate ulioshuka toka mbinguni, anayeukula hatakufa.


Mimi ni ule mukate wa uzima, ulioshuka toka mbinguni. Kama mutu akikula mukate huu ataishi milele. Na mukate nitakaotoa ni mwili wangu, utakaotolewa kusudi dunia ipate uzima.”


Huu ndio mukate ulioshuka toka mbinguni, nao si kama mukate ule babu zenu waliokula katika jangwa na kufa. Anayekula mukate huu ataishi milele.”


Kweli, kweli ninawaambia: kama mutu akishika maneno yangu, hatakufa hata milele.”


Basi sasa hakuna azabu kwa wale wanaoungana na Yesu Kristo.


Kwa maana Mungu hakututayarishia kuangamizwa kwa ukali wa kasirani yake, lakini kuokolewa kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.


Kwa njia ya Kristo, ninyi munamwamini Mungu aliyemufufua na kumupa utukufu. Na kutokana na hiyo munamwamini Mungu na kumuwekea tumaini lenu.


Ninyi ambao kwa imani munalindwa salama kwa nguvu za Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa kwa mwisho wa nyakati.


Sisi tunajua kwamba tumeponyoka lufu na kupata uzima kwa sababu tunawapenda wandugu zetu. Mutu asiyekuwa na upendo ni kama mufu.


Mutu yeyote anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo, yeye ni mutoto wa Mungu; na kila mutu anayemupenda baba anamupenda mwana wake vilevile.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ